Sports
Mwanariadha Jairus Kipchoge Birech Afariki Dunia, Kenya Yaomboleza Nyota wa Steeplechase
Familia ya riadha nchini Kenya inaomboleza kifo cha mshindi wa nishani ya fedha kwenye Michezo ya Jumuiya ya Madola ya mwaka 2014, Jairus Kipchoge Birech, mmoja wa wanariadha maarufu zaidi wa mbio za kuruka viunzi na maji (steeplechase).
Birech, mwenye umri wa miaka 32, alifariki usiku wa Alhamisi baada ya kuugua kwa muda. Kulingana na kaka yake, Alex Rotich, akizungumza kwa niaba ya familia huko Kapkagaon, Nandi, nyota huyo wa zamani alitoka Kesses, Kaunti ya Uasin Gishu.
“Alianza kuugua tarehe 16 Septemba 2025, akipata maumivu makali ya mwili kabla ya kulazwa katika Hospitali ya Mafunzo na Rufaa ya Moi, Eldoret, ambako madaktari waligundua alikuwa na kifua kikuu na homa ya uti wa mgongo,” alisema Rotich.
Familia ilisema kuwa mipango ya mazishi itatangazwa baadaye. Ameacha mke na watoto wawili.
Amezaliwa Desemba 14, 1992, Birech alikuwa nguvu kubwa katika mbio za mita 3000 kuruka viunzi na maji, akiacha alama ya kudumu katika jukwaa la kimataifa.
Aliwahi kutwaa makombe mawili ya Diamond League (2014 na 2015), kushinda mashindano 10 ya Diamond League, kuchukua dhahabu kwenye Mashindano ya Afrika mjini Marrakech, pamoja na nishani ya fedha katika Michezo ya Jumuiya ya Madola na Mashindano ya Dunia ya chipukizi (U20), na pia akabeba taji la World Cup.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

