Connect with us

Sports

Mwanariadha na Bingwa wa mbio za Discovery Maryam Lufti kushiriki mbio za Sirikwa Classic wikendi hii mjini Kapseret

Published

on

Bingwa wa toleo la 35 la mbio za Discovery Cross Country zilizofanyika Eldoret, kaunti ya Uasin Gishu, Maryam Lufti Njoki, anatarajiwa kurejea katika mashindano ya Sirikwa Classic Cross Country yatakayofanyika Jumamosi, Februari 14, mwaka huu katika kijiji cha Lobo, Kapseret akilenga kuboresha nafasi yake baada ya kumaliza wa 12 mwaka 2023 aliposhiriki kwa mara ya mwisho katika uwanja huo.

Njoki, ambaye awali alijulikana kama Christine Njoki kabla ya kubadili uraia na kuwakilisha Qatar, amesema kurejea kwake kunachochewa na nia ya kupata matokeo bora zaidi huku akiendelea kujiandaa kwa msimu wa mashindano ya uwanjani akisema ana uzoefu zaidi sasa na ana matumaini ya kuonyesha kiwango cha juu dhidi ya wapinzani wake.

Katika kitengo cha wanawake, Njoki atakumbana na ushindani mkali kutoka kwa bingwa wa dunia wa mbio za nyika Agnes Jebet Ng’etich pamoja na mshindi wa medali ya fedha ya dunia kutoka Uganda, Joy Cheptoyek.

Wengine watakaoshiriki ni pamoja na Catherine Reline ambaye sasa anawakilisha Uturuki kwa jina la Can, wanariadha wengine kutoka Uganda na Tanzania pia wanatarajiwa kushiriki katika mbio za kilomita 10 kwa wanawake.

Kwa upande wa wanaume, Mjerumani Hendrik Pfeiffer atarejea kushiriki mashindano hayo, Mykola Nyzhnyk wa Ukraine, Tshepo Mphulanyane wa Afrika Kusini na Leonard Ndiema wa Uganda miongoni mwa washindani wa kimataifa.

Mashindano hayo yanatarajiwa kuwa ya ushindani mkubwa huku wanariadha wakitumia kama sehemu ya maandalizi ya mashindano makubwa yajayo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Sports

Bingwa wa dunia mbio za mitaa 1500 Faith Kipyegon ateuliwa kuwania tuzo za kila mwaka za ‘Laureus World Sportswoman of the Year.’

Published

on

By

Nyota wa mbio za masafa ya kati kutoka Kenya, Faith Kipyegon, amepata uteuzi wake wa tatu mfululizo kuwania tuzo ya Mwanamichezo Bora wa Kike wa Mwaka katika hafla maarufu ya Laureus World Sports Awards, hatua inayozidi kuthibitisha ubabe wake katika kizazi hiki cha wanariadha.

Tuzo hizo, zinazotambuliwa kimataifa kama “Oscars za Michezo”, huandaliwa na Laureus Sport for Good Foundation na hulenga kutambua mafanikio ya kipekee, uthabiti na mchango chanya wa michezo duniani.

Uteuzi wa Kipyegon kwa miaka mitatu mfululizo unaonyesha si tu kipaji chake, bali pia uimara wa kiwango chake cha juu kwa muda mrefu. Mwaka 2024 aliteuliwa baada ya msimu wa kihistoria wa 2023 ambapo alivunja rekodi tatu za dunia na kushinda dhahabu mbili katika Mashindano ya Dunia.

Mwaka 2025 alirejea tena kwenye orodha ya wateule kufuatia mafanikio makubwa katika Michezo ya Olimpiki ya Paris, ambako aliweka historia kwa kuwa mwanamke wa kwanza kushinda medali tatu za dhahabu mfululizo katika mbio za mita 1,500.

Sasa mwaka 2026, anawania tuzo hiyo tena baada ya kuvunja rekodi yake mwenyewe ya dunia ya mita 1,500 na kutwaa taji lake la nne la dunia katika msimu bora wa 2025.

Katika kinyang’anyiro cha mwaka huu, Kipyegon anakutana na ushindani mkali kutoka kwa nyota wengine wa kimataifa akiwemo Sydney McLaughlin-Levrone, Melissa Jefferson-Wooden, Aitana Bonmati, Aryna Sabalenka, na Katie Ledecky.

Uteuzi huu unaendeleza hadhi ya Kipyegon kama mmoja wa wanariadha bora zaidi duniani na fahari kubwa kwa Kenya katika jukwaa la kimataifa.

Continue Reading

Trending