Connect with us

Sports

Napoli yatangaza kumsajili Rasmus Hojlund kwa mkopo kutoka Manchester United

Published

on

Kilabu ya Napoli hapo jana imetangaza kumsajili mshambuliaji Rasmus Hojlund kwa mkopo kutoka kilabu ya Manchester United ikiwa na wajibu wa kumnunua kwa mkataba wa kudumu, hatua inayomaliza kipindi chake kigumu kwenye klabu ya Old Trafford.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Uingereza, Napoli italipa pauni milioni 38 (sawa na dola milioni 51.5) kwa mkataba wa kudumu wa Hojlund msimu ujao.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 raia wa Denmark alisajiliwa na United akitokea Atalanta miaka miwili iliyopita, lakini alihangaika kuthibitisha thamani ya ada yake ya pauni milioni 64 kwenye kikosi kilichokuwa kinakosa ufanisi. Alifunga mabao 26 katika mechi 95 za mashindano yote akiwa na miamba hiyo ya Ligi Kuu ya England, lakini aliachwa nje na kocha Ruben Amorim kabla ya kuanza kwa msimu huu.

Hojlund alipata wakati mgumu katika ligi ya Uingereza msimu uliopita, akifunga mabao manne pekee katika mechi 32, japokuwa alifunga mara sita katika safari ya United kufika fainali ya Europa League.

Napoli walihitaji mshambuliaji mpya baada ya Romelu Lukaku kujeruhiwa paja wakati wa maandalizi ya msimu, huku vyombo vya habari vya Italia vikidai anaweza kuwa nje hadi mwaka 2026.

Hojlund aliwahi kucheza Italia na Atalanta, akifunga mabao 10 katika mechi 34.

Kikosi cha Antonio Conte, Napoli, kilitwaa Scudetto kwa tofauti ya alama moja mbele ya Inter Milan msimu uliopita.

Napoli wameanza vyema kampeni ya kutetea ubingwa, wakishinda mechi zao mbili za mwanzo huku usajili wao mpya wa kiangazi Kevin De Bruyne akionyesha kiwango cha kuvutia.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending