Sports
Omanyala Amaliza Wa Tatu Mjini Rome
Mkenya na bingwa wa Bara Afrika Ferdinand Omanyala ameweza kumaliza wa tatu mbio za msururu wa Diamond Ligi mjini Rome Italia usiku wa kuamkia leo.
Omanyala alitumia muda wake bora wa sekunde 10.01 nyuma ya mwamerika Trayvon Brommel aliyemaliza wa kwanza kwa kutumia sekunde 9.84 naye Emmanuel Eseme wa Cameroon akimaliza nafasi ya tatu na 9.99.
Haya yanajiri siku chache tu baada ya bingwa huyo kumaliza tena nafasi ya tatu mashindano ya Kip Keino Classic jijini Nairobi.
katika mbio zingine Mkenya Beatrice Chebet alikimbia mbio za kasi zaidi wa dakika ya 14.03.69 na kushinda mbio za mita 5000 ikiwa ni muda bora zaidi mwaka huu akiwapiku wenzake Freweyni Hailu (Ethiopia) na Nadia Battocletti (Italy.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

