Sports
Police Bullets Kuanza kampeni ya CECAFA kwa matarajio ya kutwaa ubingwa
Mkufunzi wa kilabu ya Kenya Police Bullets, Beldine Odemba, amesema timu yake iko tayari kupambana hadi mwisho na kutwaa ubingwa wa CECAFA Qualifiers za Ligi ya Mabingwa wa Wanawake wa CAF.
Mabingwa wa FKF Women’s Premier League wataanza kampeni yao siku ya hapo kesho, Septemba 4, 2025, dhidi ya Kampala Queens ya Uganda katika Uwanja wa Nyayo National Stadium. Wapo Kundi A, ambalo pia linajumuisha Denden FC ya Eritrea.
Kundi B lina mabingwa watetezi Commercial Bank of Ethiopia (CBE), pamoja na Top Girls Academy ya Burundi na Rayon Sports WFC ya Rwanda.
Kundi C linaongozwa na JKT Queens ya Tanzania, wakijiunga na Yei Joint Stars ya Sudan Kusini na JKU Princess ya Zanzibar.
“Wasichana wako tayari kabisa kuanza mashindano ya CECAFA.wamepata mafunzo makali na naamini faida ya kucheza nyumbani itatufanikisha kutwaa taji na kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa wa Wanawake wa CAF. Kama nilivyosema awali, tutaheshimu kila timu na hatuwezi kuidharau timu yoyote,” alisema Odemba.
Mwalimu huyo akiwahimiza mashabiki kujitokeza kwa wingi katika viwanja vya Nyayo Stadium na Ulinzi Complex kuwashangilia Bullets.
Kwa Police Bullets, dhamira ni ya kulipiza kisasi.
Mwaka jana mjini Addis Ababa, walikaribia kufuzu lakini wakapoteza 1-0 dhidi ya CBE kwenye fainali. Safari hii, wamedhamiria kutumia nafasi yao ipasavyo wakiwa nyumbani.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

