Connect with us

Sports

Rais Ruto apongeza kilabu ya Nairobi United baada ya kufuzu Makundi kombe la Mashirikisho barani Afrika

Published

on

Rais William Ruto amepongeza klabu ya Nairobi United Football Club kwa kuandika historia kwa kufuzu kwa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho la CAF (CAF Confederation Cup) kwa mara ya kwanza katika historia yake.

Rais Ruto alieleza mafanikio hayo kama “wakati wa fahari kubwa ya kitaifa” na ushahidi wa ukuaji wa hadhi ya Kenya katika soka la Afrika.

“Hii ni hatua ya kipekee, iliyojengwa kwa ujasiri, nidhamu na uvumilivu usioyumba. Ushindi huu umechochea ari ya taifa letu na kuthibitisha nafasi halali ya Kenya katika ramani ya soka la Afrika,” alisema Rais Ruto katika taarifa yake.

Kevin Oduor alijitokeza kuwa shujaa wa mechi hiyo baada ya Nairobi United kuishinda Etoile Sportive du Sahel ya Tunisia kwa mikwaju ya penalti 7-6, na hivyo kufuzu kwa hatua ya makundi ya michuano hiyo ya kifahari Jumapili usiku.

Kipa huyo aliokoa penalti mbili muhimu wakati Naibois (jina la utani la timu hiyo) waliandika historia kwa kufuzu kwa mara ya kwanza katika hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho.

Wawakilishi hao wapya wa Kenya barani Afrika walikuwa na faida ya mabao 2-0 kutoka mechi ya kwanza jijini Nairobi, lakini wenyeji walirejesha matokeo kwa ushindi wa 2-0 katika muda wa kawaida, na hivyo kufanya jumla ya 2-2, kabla ya pambano kuamuliwa kwa mikwaju ya penalti.

Kwa kufuzu kwa hatua ya makundi, Nairobi United watavuna takriban Shilingi milioni 51 kama zawadi kutoka CAF.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Sports

Bingwa wa dunia mbio za mitaa 1500 Faith Kipyegon ateuliwa kuwania tuzo za kila mwaka za ‘Laureus World Sportswoman of the Year.’

Published

on

By

Nyota wa mbio za masafa ya kati kutoka Kenya, Faith Kipyegon, amepata uteuzi wake wa tatu mfululizo kuwania tuzo ya Mwanamichezo Bora wa Kike wa Mwaka katika hafla maarufu ya Laureus World Sports Awards, hatua inayozidi kuthibitisha ubabe wake katika kizazi hiki cha wanariadha.

Tuzo hizo, zinazotambuliwa kimataifa kama “Oscars za Michezo”, huandaliwa na Laureus Sport for Good Foundation na hulenga kutambua mafanikio ya kipekee, uthabiti na mchango chanya wa michezo duniani.

Uteuzi wa Kipyegon kwa miaka mitatu mfululizo unaonyesha si tu kipaji chake, bali pia uimara wa kiwango chake cha juu kwa muda mrefu. Mwaka 2024 aliteuliwa baada ya msimu wa kihistoria wa 2023 ambapo alivunja rekodi tatu za dunia na kushinda dhahabu mbili katika Mashindano ya Dunia.

Mwaka 2025 alirejea tena kwenye orodha ya wateule kufuatia mafanikio makubwa katika Michezo ya Olimpiki ya Paris, ambako aliweka historia kwa kuwa mwanamke wa kwanza kushinda medali tatu za dhahabu mfululizo katika mbio za mita 1,500.

Sasa mwaka 2026, anawania tuzo hiyo tena baada ya kuvunja rekodi yake mwenyewe ya dunia ya mita 1,500 na kutwaa taji lake la nne la dunia katika msimu bora wa 2025.

Katika kinyang’anyiro cha mwaka huu, Kipyegon anakutana na ushindani mkali kutoka kwa nyota wengine wa kimataifa akiwemo Sydney McLaughlin-Levrone, Melissa Jefferson-Wooden, Aitana Bonmati, Aryna Sabalenka, na Katie Ledecky.

Uteuzi huu unaendeleza hadhi ya Kipyegon kama mmoja wa wanariadha bora zaidi duniani na fahari kubwa kwa Kenya katika jukwaa la kimataifa.

Continue Reading

Trending