Sports
Rais wa JKA Kenya Wakili George Kithi atangaza udhamini kamili kwa Wanakarate wa Kilifi
Rais wa Japan Karate Association Kenya, wakili George ametangaza kuwa mdhamini mkuu wa timu za Karate kutoka Kilifi kushiriki katika Mashindano ya Desemba yajayo.
Mashindano ya Desemba yatatumika kama mashindano rasmi ya kuchagua timu ya taifa itakayoshiriki kwenye Kombe la Dunia la JKA,”Tumejitolea kuhakikisha kwamba kila kanda inapata nafasi ya kuonyesha wapiganaji wake bora, na kwamba hakuna kipaji kinachopuuzwa kwa sababu ya changamoto za kifedha. Kwa kudhamini timu hizi, tunalenga kusawazisha uwanja wa mashindano na kuhamasisha wakarateka wachanga kote nchini kujitahidi zaidi, kuwa na ndoto kubwa na kuamini katika uwezo wao,” amesema Wakili.
“Ninaziita dojo zote, wakufunzi na wakarateka wote kujiandaa kwa nidhamu na shauku. Haya si mashindano tu hii ni nafasi ya kuvaa rangi za taifa kwa fahari na kuonyesha ulimwengu nguvu, ustadi na roho ya Karate ya Kenya.”
“Tushirikiane wote huko Kilifi kuandika historia na kuweka viwango vipya vya ubora katika sanaa ya mapigano hayo.”
Mashindano hayo yatafanyika jijini Nairobi ugani Nyayo.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

