Connect with us

Sports

Sinner na Alcaraz Wakutana Tena Fainali ya US Open Baada ya Muitaliano Kufuzu Fainali ya Tano Mfululizo ya Grand Slam

Published

on

Bingwa taji la US Open mchezo wa tenisi Jannik Sinner anatarajia mechi ya kipekee na “maalum” atakapokutana na mchezaji wa pili duniani Carlos Alcaraz raia wa Uhispania kwenye fainali ya wanaume ya US Open baada ya Muitaliano huyo kufuzu kwa fainali yake ya tano mfululizo ya Grand Slam siku ya Ijumaa.

Sinner alimshinda Felix Auger-Aliassime kwa seti 6-1, 3-6, 6-3, 6-4 na sasa analenga taji lake la tano la Grand Slam baada ya kujiunga na Rod Laver, Roger Federer na Novak Djokovic kama wanaume pekee kufika fainali zote nne za Grand Slam katika msimu mmoja.

“Nadhani kufika fainali tano mfululizo za Grand Slam ni jambo kubwa. Uthabiti na kujiweka katika hatua za mwisho za mashindano makubwa tuliyonayo, ni kitu cha kushangaza,” alisema Sinner.

Nafasi yake ya kwanza duniani itakuwa hatarini Jumapili wakati atakapokutana na Alcaraz kwa mara ya tatu mfululizo katika fainali ya Grand Slam.

Sinner mwenye umri wa miaka 24 alitwaa mataji ya Australian Open na Wimbledon msimu huu lakini alifungwa na Alcaraz mwenye miaka 22 katika pambano kali la seti tano kwenye French Open.

“Uwanjani tunapenda kukutana, unajua, kwa sababu kutokana na nafasi zetu kwenye viwango, inamaanisha tunafanya vizuri kwenye mashindano,” alisema Sinner.

Watakutana tena US Open kwa mara ya pili. Mchuano wao wa kwanza ulikuwa robo-fainali ya 2022, pambano kubwa lililounda ushindani wao.

“Jumapili ni siku maalum sana na fainali ya kushangaza tena,” alisema Sinner. “Ninahisi ushindani wetu ulianza hapa kwa kucheza mechi ya ajabu. Sasa sisi ni wachezaji tofauti, wenye kujiamini zaidi pia.”

Miaka mitatu iliyopita, Alcaraz ndiye aliyeshinda baada ya pambano lililodumu saa 5 na dakika 15 na kumalizika kabla ya saa 9 alfajiri huko New York, na Mspaniola huyo akaenda kunyanyua taji lake la kwanza la Grand Slam kwenye mashindano hayo.

Sinner analenga kumshinda Alcaraz Jumapili kwa kutwaa taji lake la tano la Grand Slam. Mafanikio hayo yamejengwa zaidi kwenye ushindi wa mechi 27 mfululizo za Grand Slam kwenye uwanja wa hard court.

Analenga kuwa mwanaume wa kwanza kutetea taji la US Open tangu Federer alipochukua la mwisho kati ya mataji yake matano mfululizo mwaka 2008.

Mkanada Auger-Aliassime alikuwa akijaribu kufuzu kwa fainali yake ya kwanza ya Grand Slam baada ya kufika nusu fainali kwa mara ya kwanza tangu safari yake hadi hatua hiyo hiyo kwenye US Open mwaka 2021.

“Sina majuto. Nilicheza kwa njia yangu. Nilicheza mchezo wangu. Unajua, kwa namna fulani unaishi na kufa na maamuzi yako,” alisema Auger-Aliassime.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending