Sports
Stars Yapanda Msimamo Wa FIFA
Timu ya Taifa ya soka Harambee Stars imepanda nafasi mbili juu katika msimamo wa Shirikisho la Soka Ulimwenguni FIFA kutoka 111 hadi 109 msimamo unaotolewa kila mwezi ukiwa ni msimamo wa mwezi jana.
Stars katika kipindi hicho ilicheza mechi mbili za kirafiki wakitoka sare na badaye wakishinda taifa la Chad magoli 2-1 ,Taifa la Uganda lingali la kwanza Afrika Mashariki wakiwa nafasi ya 97.
Taifa la Morocco linashikilia nafasi ya kwanza Barani Afrika na ni ya 12 ulimwenguni wakifutwa na mataifa ya Senegal kisha Misri katika nafasi ya pili na tatu.
Mabingwa wa Dunia Argentina ni ya kwanza kote ulimwenguni likifutwa na Uhispania,Ufaransa na Uingereza,nafasi ya pili tatu na nne mtawalia.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

