Connect with us

Sports

Sudan Kuzichakaza Ndaani ya Nusu Fainali Mashindano ya CHAN

Published

on

Timu ya taifa la Sudan iliingia kwenye Mashindano ya Mataifa ya Afrika (CHAN) ikiwa haikutarajiwa kabisa kufika mbali kwani ligi yake ya nyumbani karibu haipo katika nchi iliyokumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe, na kikosi kilikuwa na siku chache tu za mazoezi ya pamoja.
Hata hivyo, Falcons of Jediane wamezipinga changamoto zote na kufika nusu fainali za CHAN, ambako timu zinaruhusiwa kuchagua wachezaji pekee kutoka ligi zao za nyumbani.

Sudan ina ligi ya ndani, lakini kwa jina tu. Sudan haijawahi kuandaa mashindano ya maana ya ligi ya ndani tangu kuzuka kwa mzozo mwaka 2023 kati ya jeshi la taifa na Kikosi cha Usaidizi wa Haraka (RSF), ambacho kimesababisha vifo vya maelfu ya watu. Vilabu viwili vikubwa zaidi nchini humo, Al Hilal na Al Merrikh, vilikuwa vinacheza takriban kilomita 5,000 magharibi katika ligi ya Mauritania.

Baada ya mapumziko mafupi ya mapigano mapema mwaka huu, vilabu hivyo viliamua kurejea na kuungana na vilabu vingine sita kuunda Sudan Elite League ya mwezi mmoja.

Ligi hiyo ndogo iliandaliwa na Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) ili kuruhusu Sudan kuchagua vilabu vitakavyoshiriki michuano ya bara msimu ujao. Pia iliunda kikosi cha CHAN.

Kikosi hicho kilikuwa na siku nne pekee za kufanya mazoezi kabla ya kuwasili CHAN, huku kocha wao kutoka Ghana, James Kwesi Appiah, akieleza waziwazi hofu kwamba wachezaji wake wasingeweza kushindana ipasavyo kutokana na mazoezi haba.

Lakini timu hiyo ilipata njia ya kupenya—wakitoa sare mara mbili na kisha kuivunja Nigeria 4-0 na kufuzu kileleni mwa kundi lao.

Mchezo wao wa robo fainali dhidi ya Algeria pia ulimalizika kwa sare lakini Sudan ilishinda 4-2 kupitia mikwaju ya penalti.

Vilabu viwili vilivyofanikiwa zaidi nchini humo, Al Hilal na Al Merrikh, vilikuwa vinacheza takribani kilomita 5,000 magharibi katika ligi ya Mauritania.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending