Sports
Timu Ya Soka Harambee Stars yashuka nafasi mbili msimamo wa dunia wa FIFA
Timu ya taifa ya soka ya Kenya, Harambee Stars, imeshuka kwa nafasi mbili kwenye msimamo wa Dunia FIFA wa mwezi huu uliotolewa leo.
Kenya ni ya 112 mwezi Septemba kutoka nafasi ya 110 iliyokuwa ikishikilia mwezi Agosti.
Harambee Stars imeshuka baada ya kushindwa na Gambia kwa mabao 3-1, katika mechi ya kundi F kufuzu kwa Kombe la Dunia mapema mwezi huu.
Uganda ni ya kwanza Afrika Mashariki, ikishikilia nafasi ya 82 kati ya 84 ya mwezi jana, ikifuatwa na Tanzania katika nafasi ya 117.
Morocco ingali ya kwanza Afrika ikiwa ya 13, ikifuatwa na Senegal katika nafasi ya 18 huku Misri ikiwa ya 35.
Uhispania imechupa hadi nafasi ya kwanza ikifuatwa na Ufaransa huku mabingwa wa Dunia Argentina wakishuka hadi nafasi ya tatu.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

