Connect with us

Sports

Timu ya Taifa ya Kenya ya Para Air Badminton yashinda wenyeji Uturuki, yajikatia tiketi ya fainali

Published

on

Timu ya taifa ya Kenya ya Para Air Badminton iliibuka na ushindi mnono dhidi ya Uturuki A kwa alama 3–0 katika kipengele cha Mixed Triples na pia ikaishinda Uturuki 2 katika Mixed Triples Relays wakati wa Mashindano ya Dunia ya Michezo ya Uwezo (World Ability Sports Beach Games) yanayoendelea katika ufuo wa Pompei, Mersin, Uturuki siku ya Jumatano. Ushindi huo uliihakikishia Kenya tiketi ya kucheza fainali siku ya Alhamisi na Ijumaa mtawalia.

Akizungumza baada ya mechi, kocha mkuu John Mburu alionyesha furaha kubwa kutokana na matokeo hayo, lakini alilalamikia changamoto ya ukosefu wa lugha ya kimataifa inayowaunganisha wageni.

“Waamuzi wanazungumza Kituruki, bahati nzuri mmoja wa wachezaji wetu, Nicholas Keiyo, anaelewa lugha hiyo. Hilo limetusaidia sana kufanikisha ushindi huu,” alisema Mburu, ambaye aliwateua Benson Nduva, Caleb Omollo, Mary Nduku, Patrick Mwema na Boniface Were kwa mechi ya robo fainali dhidi ya Uturuki 1, ambapo Kenya ilishinda 3–0.

Katika nusu fainali za Jumatano, Caleb Omollo, Patrick Mwema, Benson Nduva, Mary Nduku na Boniface Were waliichapa Uturuki 2 iliyokuwa na Sükrü Gül, Cemre Gül Arïn na Fuhat Soruklu, katika mchezo mkali uliomalizika kwa ushindi wa 3–0 kwa Kenya, na hivyo kufuzu fainali ya Ijumaa.

Jioni ya Jumatano, Kenya ilijiandaa kwa pambano la Mixed Triples Relays, mbio za kusisimua ambapo timu hufukuzia kufikisha alama 60, kila robo ikiwa na alama 15, na kila timu ikiwa na wachezaji sita.

Timu ya Kenya A chini ya Mburu iliwajumuisha Mary Nduku, Benson Nduva na Caleb Omollo, huku Nicholas Keiyo, Elizabeth Nabwire na Patrick Mwema wakiwa wachezaji wa akiba, walipokutana na Ali Altiparmak, Burak May, Iremnur Yazgan, Mustafa Tugra na Sedat Tumkaya wa Uturuki 1.

Kenya ilianza vizuri kwa kufungua pengo kubwa — Kenya 56 dhidi ya Uturuki 29 — lakini wenyeji wakapunguza pengo hilo, na Burak May kufunga kwa sekunde za mwisho kuwapa ushindi wa 60–59, licha ya juhudi za Patrick Mwema kuokoa mchezo huo.

Katika mchezo mwingine, Kenya B iliyoongozwa na Newton Gatobu, Japheth Kaikai, Ashley Autai, Boniface Were, Petronila Muhani na Martin Gikonyo ilipoteza 42–60 dhidi ya timu ya mchanganyiko ya Bahrain/Uturuki iliyokuwa na Ahmed Abuseter, Kerim Kíyak, Zeinab Ali, Sukru Gul na Elfi Dokuzluoglu.

Tegemeo la mwisho la Kenya lilikuwa Kenya A kurejea kwa mchezo wa lazima kushinda dhidi ya Uturuki 2. Kwa kutumia uzoefu na mbinu zake, Kocha Mburu aliwapanga nyota wake bora — Benson Nduva, Caleb Omollo na Elizabeth Nabwire — katika robo ya mwisho iliyokuwa na mvutano mkubwa hadi sekunde za mwisho. Kenya ilishinda 60–50, ikiwanyamazisha wenyeji waliokuwa wakishangilia.

Kwa ushindi huo, matumaini ya Kenya ya kupata medali katika Air Para-Badminton Mixed Triples Relays na Mixed Triples yako hai, huku timu mbili zikijihakikishia nafasi katika fainali za Alhamisi na Ijumaa.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending