Connect with us

Sports

Uingereza yawapa wapinzani onyo baada ya kuichapa Serbia 5-0, Haaland apiga mabao matano kwa Norway

Published

on

Timu ya taifa la Uingereza ilituma onyo kali kwa wapinzani wao wa Kombe la Dunia baada ya kuifumua Serbia 5-0 katika mchezo wa kufuzu siku ya Jumanne, huku Erling Haaland akifunga mabao matano na kuisaidia Norway kuendeleza rekodi ya ushindi wa asilimia 100.

Kwingineko barani Ulaya, Ureno na Ufaransa ziligeuza matokeo baada ya kuwa nyuma na kupata ushindi wa pili mfululizo katika harakati zao za kufuzu kwa michuano ya mwakani itakayofanyika Marekani, Mexico na Canada.

Ubora wa kikosi cha Thomas Tuchel ulitiwa shaka baada ya ushindi hafifu wa 2-0 dhidi ya Andorra siku ya Jumamosi huko Villa Park, lakini safari hii walitoa jibu tosha.

Uingereza ilidhibiti dakika za mwanzo mjini Belgrade na kufungua ubao dakika ya 33, wakati Harry Kane alipofunga bao lake la 74 la kimataifa kwa kichwa akimalizia kona ya Declan Rice. Wageni waliongeza bao dakika mbili baadaye, Noni Madueke akimalizia pasi nzuri ya kichwa kutoka Morgan Rogers na kumchambua kipa wa Serbia, Djordje Petrovic.

Bao la tatu lilipatikana dakika ya 52, Ezri Konsa akipiga shuti kufuatia mpira uliorudi baada ya adhabu ndogo na kufunga bao lake la kwanza la kimataifa.

Mpira mwingine wa adhabu uliopigwa na Rice ulipelekea bao la nne, Marc Guehi akiteleza na kufunga kufuatia faulo iliyofanywa dhidi ya Kane na Nikola Milenkovic, ambaye alionyeshwa kadi nyekundu moja kwa moja.

Mbadala Marcus Rashford alifunga kwa mkwaju wa penalti mwishoni na kukamilisha usiku bora kwa Uingereza.

Uingereza sasa inaweza kufuzu kwa Kombe la Dunia kwa mara ya nane mfululizo kwenye mchezo wao ujao wa Kundi K dhidi ya Latvia mwezi ujao.

Katika mechi nyingine ya kundi hilo, Albania ilipanda hadi nafasi ya pili baada ya kuishinda Latvia 1-0 jijini Tirana.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending