Connect with us

Sports

Ujenzi wa Uwanja mpya wa Voliboli waanza Kilifi, Huku Ujenzi wa uwanja wa mpira wa vikapu ukikaribia kukamilika

Published

on

Vijana na wapenzi wa mchezo wa Voliboli Kilifi sasa wana kila sababu ya kutabasamu baada ya kilio chao cha kupata uwanja mpya kuonekana kujibiwa hivi karibuni.

Kulingana na mwanakandarasi mkuu wa ujenzi wa uwanja huo Athman Muhaji ni kwamba zaidi ya shilingi milioni 1.5 imetengwa kwa ajili ya ujenzi wa uwanja huo mpya ikiwa ni zaidi ya laki mbili kwa fadha zilizotumika kujenga uga wa Basketiboli ugani Karisa Maitha.

“Kama huu mradi kuisha itagharimu kama shilingi milioni 1.6 ama 1.4 hivi ili kupata uwanja bora mno naamini uwanja huo utaisha kwa kipindi cha wiki mbili hivi.”

Kwa Upande wake katibu mkuu mwandalizi wa chama cha Voliboli kaunti kilifi Henry Nyambu amekaribisha kwa moyo mkunjufu hatua hiyo mpya akikiri kwa muda na miaka mingi wamecheza kwenye vumbi na kuona uwanja mpya unajengwa ni jambo la kutia moyo akimpongeza mbunge wa Kilifi Kaskazini Owen Baya.

“Kuona mweshimiwa anajenga uwanja wa kimataifa wa Voliboli hakika ni fahari lakini pia ni historia kwani hata kwa kaunti zingine na wapinzani wetu hawana viwanja vya haina hii kwa hiyo nimshukuru saana mheshimiwa kwa kazi hii kuntu,naamini itakua ni uwanja wa Ubora zaidi ya kujivunia kama wanakilifi.”

Kulingana na mshirikishi wa Sokoni Ward Johnson Charo ni kwamba huu ni mwamko mpya Kilifi kwani viwanja vya aina hii vimekua nadra mno kuzipata na sasa ni fahari ya kila kijana kutumia vipaji vyao vilivyo katika michezo hiyo.

“Kwa Muda vijana wamekua wakicheza katika viwanja vya vumbi ila sasa ni mwamko mpya kweli kweli kuendeleza kuonyesha vipaji vyao katika viwanja vyenye ubora.”

Haya yanajiri huku uwanja mpya wa mpira wa vikapu ukikamilisha katika uwanja huo uo zote kwa ufadhili wa mbunge wa Kilifi Kaskazini Owen Baya.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending