Sports
United Wamewasilisha Ofa Kumsajili Mbeumo
Kilabu ya Manchester United imewasilisha ofa ya pauni milioni 55 kwa kilabu ya Brenford kuhusiana na uhamisho wa winga matata Bryan Mbeumo raia wa Cameroon.
Hata hivyo ofa hiyo inatarajiwa kukataliwa na Brenford ambao wanataka pauni milioni 60 kumwachilia mchezaji huyo ambaye aliwasaidia pakubwa msimu ambao umekamilika.
Mchezaji huyo mwneye umri wa miaka 26 ameambia United anataka mshahara wa kitita cha pauni laki 250,000 kila wiki ili aweze kutua OLd Trafford licha ya kulipwa pauni Elfu 50 kila wiki na Brenford.
Mbeumo alifunga magoli 20 msimu ambao umekamilika na kuchangia mengine 9 na kusaidia The Bees kumaliza ya 10 ligi ya Epl na licha ya kumezewa mate na vilabu vya Arsenal,Newcastle United amesema chaguo lake la kwanza na kutua Old Trafford msimu ujao.
Iwapo United watapata sahihi yake basi atakua sajili wa pili kwa kocha Ruben Amorim baada ya kupata mshambulizi Matheus Cunha.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

