Connect with us

Sports

US Open: Jannik Sinner aingia raundi ya tatu, Wong aandika historia kwa Hong Kong

Published

on

Bingwa mtetezi wa wanaume mpira wa tenesi Jannik Sinner aliingia raundi ya tatu ya US Open hapo jana huku Coco Gauff na Iga Swiatek wakipambana kuendeleza ndoto zao za kutwaa ubingwa.

Sinner alimfagia Mwaustralia Alexei Popyrin kwa seti 6-3, 6-2, 6-2 na kuongeza rekodi yake ya ushindi katika michuano ya Grand Slam kwenye uwanja mgumu hadi mechi 23 mfululizo.

Mchezaji huyo namba moja kwa kupanda viwango kutoka Italia ameanza kwa kishindo katika azma yake ya kuwa mwanaume wa kwanza kutetea taji la US Open tangu Roger Federer aliposhinda mara tano mfululizo kati ya 2004–2008.
“Ninalenga kuboresha huduma (serve), lakini mengine najihisi vizuri,” alisema Sinner.

Sasa Sinner atakutana na mchezaji wa Kanada namba 27 kwa viwango, Denis Shapovalov, katika raundi ya tatu siku ya Jumamosi.

Tayari amefika fainali ya Grand Slam zote tatu msimu huu, akitwaa Australian Open na Wimbledon, huku akikubali kichapo kutoka kwa Carlos Alcaraz kwenye French Open.

Mshindi namba tatu kwa viwango bora Alexander Zverev alishinda kirahisi 6-4, 6-4, 6-4 dhidi ya Mbritania Jacob Fearnley, huku Lorenzo Musetti akimnyamazisha Mbelgiji David Goffin.
Mchezaji namba 15 kwa viwango kutoka Urusi Andrey Rublev alimshinda Tristan Boyer wa Marekani (wild card) kwa seti nne, na sasa ataumana na kijana wa Hong Kong Coleman Wong katika hatua ya 32 bora.

Wong, mwenye umri wa miaka 21 na aliyefuzu kupitia mashindano ya awali, aliendeleza hadithi yake ya kusisimua New York kwa kumshinda Mwaustralia Adam Walton 7-6 (7/5), 6-2, 4-6, 6-4.

Wong, anayerankiwa namba 173 duniani, tayari aliweka historia mapema wiki hii kwa kuwa mwanaume wa kwanza kutoka Hong Kong kushinda mechi ya Grand Slam ya mchuano wa mtu mmoja.
“Hii ni ndoto yangu, kitu ambacho kila mchezaji wa tenisi huota — kuendelea kupiga hatua kwenye Slam,” alisema Wong.

Katika mechi ya mwisho ya siku, Mmarekani mchezaji namba 14 Tommy Paul hatimaye alimshinda Mreno Nuno Borges saa 7:46 usiku katika pambano la seti tano kali.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending