Sports
Wanariadha Kuvuna Panono Wakishinda Dhahabu Olimpiki
Serikali kupitia kwa Wizara ya Michezo imedokeza kwamba wanariadha wote wanaovunja rekodi na kufanya vizuri mashindano ya Olimpiki watavuna vinono haya ni kwa mujibu wa Waziri wa Michezo Salim Mvurya.
Waziri huyo aliyasema hayo wakati wa kupokea wanariadha bingwa wa olimpiki mita 1500 Faith Kipyegon na bingwa wa mitaa 5000 Beatrice Chebet baada ya kurejea nchini kutoka Eugene Oregon Marekani.
Kwa mujibu wa Mvurya mshindi wa tuzo la dhahabu Olimpiki sasa atakakua anapokea milioni 3 kutoka laki 750 huku mshindi wa fedha akipokea milioni 2 kutoka laki 500,000 naye wa shaba milioni moja.
Mwanariadha Kipyegon akivunja rekodi yake ya mitaa 1500 kwa muda wake bora wa dakika 3:48.68 huku Chebet akivunja rekodi kwa muda wa dakika 13:58.06.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

