Sports
Wanyonyi Kuongoza Wakenya Katika Mashindano ya Diamond League Lausanne
Bingwa wa Olimpiki wa mbio za mita 800 kutoka Kenya, Emmanuel Wanyonyi, ataongoza kikosi thabiti cha Wakenya katika mashindano ya Athletissima Diamond League yatakayofanyika Lausanne, Uswizi, Jumatano.
Wanyonyi amekuwa mwanariadha bora zaidi wa mbio za kati mwaka 2024, akishiriki kwa uthabiti tangu Februari na kushinda kwa kishindo mjini Oslo, Stockholm, Monaco, na London.
Muda wake wa 1:41.44 alioukimbia mjini Monaco ndio muda bora zaidi duniani msimu huu. Lausanne pia si uwanja mgeni kwa kijana huyo mwenye umri wa miaka 20, kwani ni hapa mnamo 2024 alipoweka rekodi yake ya maisha ya 1:41.11 — muda wa tatu wa haraka zaidi katika historia.
Fainali ya wanaume mita 800 mjini Lausanne inatarajiwa kuwa ya kuvutia sana, huku Wanyonyi akikabiliana na bingwa wa dunia Marco Arop, bingwa wa Ulaya Gabriel Tual, na bingwa wa dunia wa ndani ya ukumbi Bryce Hoppel.
Kenya pia itawakilishwa vyema katika mbio za mita 5000 za wanaume, ambapo aliyewahi kushinda medali ya fedha ya ubingwa wa dunia Jacob Krop atakabiliana na wapinzani wakali akiwemo Muethiopia Hagos Gebrhiwet, Mbahareni Birhanu Balew, na Mmarekani Grant Fisher.
Kwa vile mashindano ya hivi karibuni ya Diamond League yamezalisha muda chini ya dakika 12:50, mbio hizi zinatarajiwa kuwa na msisimko mkubwa.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

