Sports
Waziri Wa Usalama Murkomen Asema Tuko Tayari Chan
Waziri wa Usalama wa ndaani Kipchumba Murkomen amesema kwamba Taifa la Kenya liko tayari kwa kipute cha CHAN mwezi ujao.
Akizungumza na wanahabari hapo jana Murkomen amesema miondo misingi ya usafiri na usalama iko tayari kwa sasa wakiwa tayari kulinda usalama wa timu zote na mashabiki nje na ndaani ya uwanja.
Murkomen pia amerai mashabiki kufika uwanjani kumiminika katika viwanja mbalimbali kupiga jeki kikosi cha Stars kuweza kufanya kweli kama mchezaji wa 12.
“Viwanja vya viko tayari hata zile za mazoezi kwa ajili ya Taji hili Spesheli,tuko tayari kulinda timu zote na wachezaji pamoja na mashabiki watakao kuja nchini kushabikia timu zao nchini,Pia Nichukue fursa kurai Wakenya kujitokeza kwa wingi kuwa mtu wa 12 kushabikia vijana wa nyumbani Harambee Stars.
Kwa mujibu wa Murkomen viwanja vyote vitakavyotumika vina usalama mkubwa na wanamikakati ya kuzuia tukio lolote ambalo linaweza tokea kwenye kipute hicho kwani wamejipanga vyema kabisaa.
Kombe hilo linangoa nanga Agosti 2 uwanjani Benjamin Mkapa nchini Tanzania.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

