Sports
Zaidi ya Wachezaji 200 Waungana Railways Golf Club kwa Mashindano ya KCB East Africa Golf Tour 2025
Uwanja wa Gofu wa Railways (Par 72) unatarajiwa kuwapokea zaidi ya wachezaji 200 wa gofu kwa awamu ya kumi na nane ya Mashindano ya KCB East Africa Golf Tour 2025 siku ya Jumamosi.
Baada ya tamasha la kuvutia lililofanyika wikendi iliyopita kule Sigona, mashindano haya ya kanda yanatarajiwa kuanza mapema saa 12:30 asubuhi kwa raundi ya kwanza, kabla ya raundi ya mchana itakayoanza saa sita kamili mchana.
Akizungumza kabla ya mashindano haya, Nahodha wa Railways Golf Club, John Kamenyi, alisema wanatarajia idadi kubwa ya washiriki Jumamosi. “Mfululizo huu umekuwa muhimu sana katika kuwapa maelfu ya wapenzi wa gofu nafasi ya kuboresha ujuzi wao na pia kufurahia mchezo huu. Tumefanya kazi kubwa kuhakikisha uwanja uko katika hali bora, kwa hivyo wachezaji watarajie burudani ya hali ya juu,” alisema Kamenyi.
Hadi sasa, Mashindano ya KCB East Africa Golf Tour 2025 yamehusisha zaidi ya wachezaji 2,000 kutoka ukanda wa Afrika Mashariki na zaidi ya watoto 1,000 kupitia kliniki za golf zinazofanyika sambamba na mashindano haya.
Hapa nchini Kenya, mashindano haya tayari yamefanyika katika kaunti 10 ikiwemo Nairobi, Nakuru, Kisumu, Laikipia, Nandi, Mombasa, Kisii, Kiambu, Machakos na Kericho.
Katika nje ya nchi, mashindano hayo yamefanyika Uganda na Burundi, huku Tanzania na Rwanda zikitarajiwa kuwa wenyeji kabla ya fainali kuu kufanyika.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

