Sports
Crystal Palace Mabingwa Ngao La Jamii
Kilabu ya Crystal Palace ndio mabingwa wa taji la Ngao ya Jamii marufu kama FA Cup Community Shield mechi iliopigwa hapo jana ugani Wembley.
Haya yanajiri baada ya The Eagles kushinda magoli 3-2 kupitia mikwaju ya penalti baada ya sare ya magoli 2-2 muda wa kawaida.
The Reds walichukua uongozi kupitia kwa mshambulizi Hugo Ekitite dakika ya 4 kabila ya Palace kusawazisha kupitia kwa mshambulizi Jean Phillipe Mateta dakika ya 17 ,Hata hivyo kilabu hiyo ilichukua tena uongozi kupitia kwa beki Jeremie Frimpong dakika ya 21.
Goli la Ismael Sarr dakika ya 77 ilihakikisha mechi hiyo inamuliwa kupitia mikwaju ya penalti.
Liverpool ikipoteza penalti zake kupitia Mohammed Salah,Alexis Mc Alister,na Harvey Elliot.
Crystal walijipatia magoli yake kupitia wachezaji kwa Jean Phillipe Mateta,Ismael Sarr na Justin Devenny
The Reds wanafungua ligi kuu Uingereza Ijumaa dhidi ya Afc Bournemouth.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

