Connect with us

Sports

Kikosi cha Voliboli Chipukizi Junior Wafalme Stars watinga Nusu Fainali Mashindano ya Bara Afrika

Published

on

Timu ya taifa ya mpira wa voliboli ya vijana chini ya miaka 20, Junior Wafalme Stars, imefuzu kwa nusu fainali ya Mashindano ya Mataifa ya Afrika baada ya kuibuka na ushindi wa seti 3-1 dhidi ya Algeria katika robo fainali ya kusisimua iliyochezwa katika ukumbi wa ndani wa Hassan Mostafa mjini Giza, Misri, Alhamisi.

Kikosi kinachoongozwa na Luke Makuto kilianza kwa kusuasua, kikisalimu amri kwa Waafrika wa Kaskazini kwa seti ya kwanza 25-21, kabla ya kurejea kwa nguvu na kushinda seti ya pili na ya tatu 25-22 na 25-17 mtawalia.

Seti ya nne ilishuhudia Junior Wafalme Stars wakipambana kwa nguvu na kushinda 26-24, baada ya Waalgeria kulazimisha mchezo uendelee kwa matumaini ya kuipiku Kenya na kulazimisha seti ya maamuzi, juhudi ambazo ziligonga mwamba.

“Mchezo ulikuwa mgumu lakini ninafurahi vijana walipambana vikali na kushinda. Algeria pia ni timu nzuri na wametupa upinzani mkubwa,” alisema Njine.

Bethwel Kiplagat, aliyekuwa Mchezaji Bora Zaidi (MVP) wakati wa michezo ya mashule ya Jumuiya ya Shule za Upili Afrika Mashariki (FEASSSA), aliibuka shujaa wa mchezo huu na hadi sasa ameiwezesha Kenya kupata jumla ya pointi 102 zikiwemo mashambulizi 89.

Mshambuliaji huyo wa Shule ya Upili ya Cheptil alionekana mwenye furaha kubwa baada ya kutunukiwa tuzo ya MVP na kusaidia Junior Wafalme Stars kutinga nusu fainali.

“Ninafurahia sana kwa mchezo wa leo, ulikuwa mgumu lakini tuliweza. Tuna imani tunapoingia katika mechi ya kesho na tuko tayari kutoa makali yetu yote,” alisema.

Kenya sasa itamenyana na wenyeji Misri kesho katika nusu fainali ya kusisimua, ambapo nafasi ya kufika fainali itakuwa tiketi ya kufuzu kwa Mashindano ya Dunia ya 2028.

Awali, mechi hizi zilitarajiwa kutoa tiketi kwa Mashindano ya Dunia ya 2026, lakini yamefutwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Voliboli (FIVB) ili kupunguza msongamano wa mashindano.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending