Sports
Alcaraz,Sabalenka ndaani ya Robo Fainali,Wimbledon
Bingwa mtetezi wa Wimbledon na mchezaji anayeorodhshwa wa pili ulimwneguni kwa sasa mchezo wa Tennis Carlos Alcaraz raia wa Uhispania pamoja na Aryna Sabalenka anayeotodhshwa wa kwanza upande wa akina dada wamejitosa katika robo fainali mashindano ya Wimbledon Uingereza.
Alcaraz sasa atamenyana na Cameron Norris raia wa Uingereza akitarajiwa kuingia kwenye daftari za kumbukumbu kwa kuwa miongoni mwa wachezaji ambao wameshinda msururu huo kwa miaka mitatu mfululizo wengine ambao wamewahi kushinda mara tatu kwa mpigo ni pamoja na;Bjorn Borg, Pete Sampras, Roger Federer and Novak Djokovic.
Kwa upande wake nyota wa upande wa akina Aryna Sabalenka baada ya kushinda mechi zake zote sasa ameratibiwa kumenyana na Laura Siegemund akisaka taji la nne la Grand Slam kule Wimbledon.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

