Connect with us

Sports

Ballon d’Or Kutolea Usiku wa Leo ambapo vita ni kati ya Lamine Yamal na Ousmane Dembele

Published

on

Mshambulizi wa Paris Saint-Germain, Ousmane Dembele, anatabiriwa kumshinda nyota chipukizi wa Barcelona, Lamine Yamal, na kushinda tuzo ya Ballon d’Or  ya wanaume usiku wa leo, huku Aitana Bonmati akiwa na nafasi ya kushinda tuzo ya wanawake kwa mara ya tatu mfululizo.

Dunia ya kandanda itakutanika katika sherehe ya kifahari kwenye ukumbi wa Théâtre du Châtelet jijini Paris kubaini ni nani atakayekuwa mshindi mpya wa tuzo hii, ambayo kwa muda mrefu ilitawaliwa na Lionel Messi na Cristiano Ronaldo.

Wawili hao walishinda Ballon d’Or mara 13 kati ya mwaka 2008 hadi 2023. Tuzo hii, inayotambulika kama heshima kubwa zaidi ya mchezaji mmoja mmoja katika soka, ilikwenda kwa kiungo wa Manchester City, Rodri, mwaka jana baada ya kuiongoza Uhispania kutwaa ubingwa wa Euro 2024.

Kwa kuwa Rodri hayupo kwenye kinyang’anyiro mwaka huu baada ya kuumizwa msimu uliopita, Dembele mwenye umri wa miaka 28 ameibuka kuwa kipenzi cha mashabiki miongoni mwa orodha ya wateule wengi kutoka mabingwa wa Ligi ya Mabingwa, PSG.

Wachezaji tisa wa PSG waliotwaa ubingwa wa Ulaya baada ya ushindi wa kuvutia wa 5-0 dhidi ya Inter Milan wameorodheshwa kati ya wagombea 30.

Mbali na Dembele, wamo pia Desire Doue, Achraf Hakimi, Khvicha Kvaratskhelia, Nuno Mendes, Joao Neves, Fabian Ruiz, Vitinha, na kipa Gianluigi Donnarumma (ambaye sasa yupo Manchester City).

Lakini Dembele anaonekana kuwa na nafasi kubwa zaidi baada ya msimu wa kushangaza alipopachika mabao 35, akijaza pengo lililoachwa na Kylian Mbappé aliyeondoka. Mchango wake uliisaidia PSG kushinda mataji yote ya ndani na pia kufika fainali ya Kombe la Dunia la Vilabu.

“Ilikuwa ni msimu mzuri sana na PSG. Ni heshima kubwa kuwa miongoni mwa wanaopewa nafasi ya kushinda,” Dembele aliambia Le Monde.

Wengi wa wateule kutoka PSG huenda wakakosa sherehe hiyo baada ya mechi yao dhidi ya Marseille kuahirishwa kutokana na dhoruba kusini mwa Ufaransa. Hata hivyo, Dembele, ambaye ni majeruhi, anaweza kuhudhuria.

Kwa upande mwingine, Lamine Yamal, mwenye umri wa miaka 18 pekee, amejitokeza kama kipaji kipya cha Barcelona na anaonekana kama mrithi wa Messi.

Alishinda Kopa Trophy kwa mchezaji bora mwenye umri chini ya miaka 21 kwenye gala la mwaka jana la Ballon d’Or, baada ya kuisaidia Uhispania kushinda Euro.

Yamal alifunga mabao 18 katika mechi 55 kwenye mashindano yote msimu uliopita, akisaidia Barcelona kutwaa La Liga na Copa del Rey, japokuwa walifungwa na Inter kwenye nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending