Sports
Barcelona Yamkabidhi Jezi Namba 10 Kwa Lamine Yamal
Kilabu ya FC Barcelona imemkabidhi winga matata Lamine Yamal jezi namba 10 kilabuni humo.
Jezi hilo ambalo limevaliwa na baadhi ya wakongwe kilabuni humo ikiwemo Lionel Messi na Ronaldinho imekua na kiungo Ansu Fati ambaye kwa sasa ameondoka kilabuni humo na kujiunga na Monaco ya Ufaransa.
Huku hayo yakijiri kilabu hiyo imekumbwa na wasiwasi kuhusiana na tabia ya winga huyo katika msimu huu mapumziko baada ya kanda kumuonyesha akijivinjari na mpenzi mwenye umri mkubwa na pia ukaribu wake na Neymar wakionekana maeneo tofauti wakijivinjari mpaka saa za usiku.
Mchezaji Huyo mwenye umri wa miaka 19 alijiunga na Timu hiyo kutoka kwenye Akademia ya Kilabu hiyo LA MASIA na amekua nguzo muhimu chini ya kocha Hansi Flick akiongeza kilabu hiyo kushinda taji la Laliga na Copa De La Rey.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

