Sports
CAF Imepiga Tiki Kenya Kuanda CHAN – Musonye
Shirikisho la soka Barani Afrika CAF limetupa idhini kuandaa chan haya si maneno yangu bali ya mwenyekiti wa kamati andalizi ya CHAN Nicholas Musonye.
Akizungumza na vyombo vya habari mapema leo Musonye amesema kwamba CAF wamepiga tiki kenya kwa maandalizi ya kombe hilo badaye mwezi ujao uwanjani Kasarani.
“Shirikisho la Soka CAF lina imani nasi na hivyo limetupa nafasi ya kuanda taji la CHAN mwezi ujao,kwa sasa tunaomba watu wa nchi hii na Afrika Mashariki kwa jumla waje wafurahiye mchezo wa Soka Nairobi.”
Pia Musonye amefichua kwamba kiingilio ya mechi hizo ni kama ifuatayo;
Mashabiki mashuhuri zaidi shs.1000,mshabiki Mashuhuri kulipia ada ya shilingi 500 nao wa Russia kulipia shilingi 200.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

