Sports
Haller Ajiunga Rasmi na Utrecht Baada ya Kuondoka Borussia Dortmund
Kilabu ya Borussia Dortmund ya Ujerumani imethibitisha kwamba mshambuliaji wa taifa la Ivory Coast Sebastien Haller amejiunga na klabu ya Uholanzi, Utrecht, kwa mkataba wa kudumu.
Inaripotiwa kuwa Haller amejiunga kwa uhamisho wa bure baada ya kuruhusiwa kuvunja mkataba wake na Dortmund mwaka mmoja kabla ya muda wake kuisha.
Raia huyo wa taifa la Ivory Coast mwenye umri wa miaka 31 alitumikia nusu ya pili ya msimu uliopita kwa mkopo Utrecht, klabu aliyowahi kuichezea kati ya mwaka 2015 na 2017. Kuondoka kwake kunahitimisha kipindi kigumu akiwa Dortmund.
Baada ya kusajiliwa kwa dau la euro milioni 31 ($36m) kutoka Ajax mwaka 2022, Haller aligunduliwa kuwa na saratani ya korodani wiki chache baadaye na akakaa nje kwa miezi sita akipokea matibabu.
Alikosa penalti katika siku ya mwisho ya msimu wa 2022-23 kwenye sare ya 2-2 nyumbani dhidi ya Mainz, matokeo yaliyoiwezesha Bayern Munich kutwaa ubingwa wa Bundesliga.
Hata hivyo, mshambuliaji huyo wa zamani wa West Ham na Eintracht Frankfurt ndiye aliyefunga bao la ushindi kwa Ivory Coast katika fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka jana dhidi ya Nigeria.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

