Sports
Chelsea Kumtambulisha Delap
Mshambulizi wa kilabu ya Ipswich Town na timu ya taifa Uingereza Liam Delap amekamilisha sehemu ya kwanza ya vipimo vya kimatibu anapokamilisha uhamisho wake katika kilabu ya Chelsea.
Kwa mujibu wa gwiji wa uhamisho barani ulaya Fabrizio Romano uhamisho huo ni wa pauni milioni 30 Delap akitarajiwa kumwaga wino mkataba wa miaka mitano stamford bridge.
Licha ya kumulikwa na vilabu kadha wa kadha ikiwepo Manchester United pamoja na Newcastle United Delap aliamua kwamba chaguo lake ni Chelsea msimu huu na atakua sajili wa kwanza kwa kocha Enzo Maresca.
The Blues wanatarajiwa kumtambulisha hii leo mchezaji huyo ambaye alipachika wavuni magoli 12 msimu huu na kutoa pasi mbili kwa wenzake kufunga msimu ambao umekamilika.
Vijana hao wanaaminika pia kusaka mshambulizi tajika msimu huu wakimulika mshambulizi Victor Gyokeres na Victor Osimhen inaamnika pia wanamfukuzia winga wa Bilbao Nico Williams.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

