Connect with us

Sports

Chelsea Yafunguliwa Mashtaka kwa Ukiukaji wa Kanuni 74 za Malipo kwa Mawakala

Published

on

Kilabu ya Chelsea imefunguliwa mashtaka na Shirikisho la Soka la Uingereza (FA) kwa madai ya kukiuka kanuni 74 zinazohusiana na malipo kwa mawakala kati ya mwaka 2009 na 2022.

Mashtaka hayo yanalenga zaidi matukio yaliyotokea kati ya msimu wa 2010-11 hadi 2015-16.

Ukiukaji unaodaiwa unahusu mawakala, wapatanishi na uwekezaji wa watu wa tatu kwa wachezaji.

Chelsea wamepewa muda hadi tarehe 19 Septemba kujibu mashtaka hayo.

Kuna adhabu mbalimbali zinazoweza kutolewa dhidi ya Chelsea, ikiwemo faini, marufuku ya usajili na kupunguzwa pointi. Hata hivyo, kiwango cha juu cha ushirikiano wa klabu hiyo kitapewa kipaumbele katika kuamua uamuzi wa mwisho.

Mwenye biashara wa Kirusi Roman Abramovich alikuwa mmiliki wa klabu hiyo kuanzia mwaka 2003 hadi 2022. Aliiuza Chelsea kwa muungano ulioongozwa na mwekezaji Mmarekani Todd Boehly na kampuni ya uwekezaji binafsi Clearlake Capital.

Mnamo Julai 2023, Chelsea walitozwa faini ya pauni milioni 8.6 na Uefa kwa kukiuka kanuni za Financial Fair Play kutokana na “kuwasilisha taarifa zisizokamilika za kifedha” kati ya mwaka 2012 na 2019.

Ukiukaji huo ulibainishwa na uongozi mpya wa Stamford Bridge kufuatia mauzo ya klabu hiyo mnamo Mei 2022.

Kama ilivyoripotiwa na BBC Sport mnamo Oktoba 2023, usajili uliomhusisha Samuel Eto’o na Willian ulikuwa sehemu ya uchunguzi wa Ligi Kuu ya Uingereza kuhusu ukiukaji wa kanuni za kifedha na Chelsea.

Wachezaji hao wote wawili walijiunga na klabu hiyo wakati Abramovich akiwa bado anamiliki, wakitokea klabu ya Urusi Anzhi Makhachkala mnamo mwaka 2013.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending