Sports
Cherotich Na Yavi Kuzindua Uhasama Tena,Oregon
Bingwa wa nishani ya fedha mbio za olimpiki mitaa 3000 kuruka maji na viunzi Faith Cherotich anatarajiwa tena kuzindua uhasama na bingwa wa Olimpiki raia wa Bahrain Winfried Yavi na Mganda Peruth Chemutai katika msururu wa Prefontaine Classic Diamond League kule Eugene, Oregon Marekani hapo kesho.
Raia huyo anaingia kwenye mbio hizo akiwa na mortisha ya hali ya juu baada ya kushinda Yavi katika misururu mitatu msimu huu mbio za Doha nchini Qatar,Oslo kule Norway na Brussels.
Cherotich akiwa tayari amekusanya alama 24 dhidi ya 14 ya Yavi kuelekea katika msururu mwingine mjini Monaco Ufaransa Julai 11.
Msimamo wa 2025 Wanda Diamond League – Women’s 3000m hadi sasa;
Faith Cherotich (KEN) – 24 pts
Winfred Yavi (BRN) – 14 pts
Sembo Almayew (ETH) – 12 pts
Maraw Bouzayani (TUN) – 10 pts
Peruth Chemutai (UGA) – 9 pts
Lea Meyer (GER) – 8 pts
Courtney Wayment (USA) – 7 pts
Gabrielle Jennings (USA) – 6 pts
Norah Jeruto (KAZ) – 5 pts
Lomi Muleta (ETH) – 4 pts
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

