Connect with us

Sports

Chipolpolo Ya Zambia Inazidi Kujinoa Kambini Lusaka Tayari Kwa Chan

Published

on

SIKU 11 ZIMESALIA KWA KOMBE LA CHAN KUNGOA NANGA

ZAMBIA- Chipolopolo

Hii leo tunangazia Taifa la Zambia,wanajiita Chipolopolo kwa jina la Utani,ikiwa inaorodheshwa nafasi ya 87 kote ulimwenguni na Shirikisho la Soka Ulimwenguni FIFA.

Kocha mkuu wa Kikosi hicho ni Avram Grant raia wa taifa la Israel, hata hivyo kwenye kipute cha Chan vijana hao wataongozwa na kocha wa nyumbani na mshambulizi wa zamani wa Nchanga Rangers na Power Dynamos Wedson Nyirenda.

Chipolopolo wameshiriki kombe hilo mara nne (2009, 2016, 2018, 2020) ila wameambulia patupu bila kushinda wakimaliza ya tatu katika mwaka wa kwanza wa kombe hilo mwaka 2009 nchini DR.Congo.

Timu hiyo ni mabingwa mara moja taji la AFCON wakishinda mwaka 2012 na pia ni mabingwa mara saba kombe la COSAFA ukanda wa Afrika Kusini.

Timu hiyo yenye wachezaji 32 itaongozwa na nahodha na mzee wa kazi beki wa zamani wa TP Mazembe  Kabaso Chongo ambaye kwa sasa anapiga na Kabwe Worriors ya taifa hilo.

Badhi ya nyota wengine wa kuangaziwa katika kikosi hicho ni pamoja na mshambulizi Joseph Phiri na Evans Kayombo;

GOALKEEPERS); Francis Mwansa (Zanaco), Willard Mwanza (Power Dynamos), Levison Banda (Zesco United), Charles Kalumba (Red Arrows).

(DEFENDERS); Benedict Chepeshi, Kabaso Chongo (all Zesco United), Mathews Banda, Kendrick Mumba, (both Nkana), Killian Kanguluma (Kabwe Warriors), Kebson Kamanga, Happy Nsiku (all Red Arrows), Lyson Banda (Green Buffaloes), Dominic Chanda (Power Dynamos), John Chishimba (Zanaco).

(MIDFIELDERS); Owen Tembo, Frederick Mulambia, Prince Mumba (both Power Dynamos), Kelvin Kapumbu (Konkola Blades), Wilson Chisala (both Zanaco), Philimon Chilimina (both Green Buffaloes), Rally Bwalya (Napsa Stars), Abraham Siankombo, Kelvin Kampamba (both Zesco United), Jackson Kampamba (Mutondo Stars), Kenneth Kasanga (Nkwazi), Timothy Sichalwe (Athletico), Kelvin Mwanza (Muza FC).

(STRIKERS); Andrew Phiri (MUZA), Evans Kayombo (Napsa Stars), Charles Zulu (Nkana), Joseph Phiri (Red Arrows), Kenan Phiri (Makeni All Stars).

Zambia wako kundi A pamoja na Kenya,Angola,Morocco na Dr. Congo

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending