Connect with us

Sports

Duplantis Awinda Taji la Tano Diamond League, Lyles na Tebogo Kukutana Zurich

Published

on

Mshikilizi wa rekodi ya dunia ya kuruka kwa mlingoti, Armand ‘Mondo’ Duplantis, analenga kushinda taji lake la tano mfululizo la Diamond League hii leo mjini Zurich, jiji la Uswizi linaloandaa fainali za mashindano hayo wiki mbili tu kabla ya mashindano ya dunia jijini Tokyo.

“Nalazimika kuzingatia kwa makini, siwezi kulegeza kamba,” alisema Mswidi huyo aliyezaliwa Marekani, ambaye amekuwa katika kiwango cha juu, akiweka rekodi yake ya dunia ya 13 ya mita 6.29 mjini Budapest mapema mwezi huu.

“Matumaini makubwa ni bora kuliko kutokuwa na matumaini. Ni changamoto nzuri, kwa kweli,” aliongeza akizungumzia matarajio ya mashabiki kuhusu hali ya sasa ya mashindano ya kuruka kwa mlingoti.

Lyles dhidi ya Tebogo;

Mabingwa 26 waliobakia wa Diamond League watajulikana katika ratiba ndefu kwenye Uwanja wa Letzigrund siku ya Alhamisi.

Watazamaji wataweza kushuhudia nyota wakubwa wa dunia akiwemo Noah Lyles na Letsile Tebogo, mabingwa wa Olimpiki katika mbio za 100m na 200m.

Wawili hao watakabiliana katika mbio za wanaume za 200m, ambapo Tebogo kutoka Botswana anawinda taji lake la kwanza kabisa la Diamond League, huku Mmarekani Lyles akitafuta kushinda taji hilo kwa mara ya sita, rekodi mpya.

“Kwa kuwa mbio za Weltklasse Zurich ndizo za mwisho kabla ya mashindano ya dunia, nataka kukimbia kwa kiwango cha juu kabisa,” alisema Lyles, ambaye alilazimika kuridhika na medali ya shaba katika Olimpiki za Paris kwenye mbio za 200m zilizoshindiwa na Tebogo.

Bingwa wa Olimpiki na Diamond League, Julien Alfred, pia atashiriki katika mbio za wanawake za 100m, huku nyota wa 800m Emmanuel Wanyonyi na bingwa wa kuruka viunzi vya 400m Femke Bol wakilenga kutetea mataji yao.

Wengi wa wanariadha wamefuzu kwa fainali za Diamond League kutokana na pointi walizokusanya kwenye mashindano 14 yaliyopita, huku wachache wakipata nafasi kupitia tiketi maalum za kimataifa au kitaifa.

Hata hivyo, Jakob Ingebrigtsen hatashiriki katika mbio za wanaume za 1,500m kwa angali anauguza jeraha la msuli wa paja.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending