Connect with us

Sports

Faith Cherotich Kuanza Safari ya Kutetea Taji la Diamond League Zurich Leo

Published

on

Mshindi wa nishani ya shaba ya Olimpiki, Faith Cherotich, ndiye atakayekuwa gumzo atakapoingia uwanjani mjini Zurich leo usiku akilenga kutetea taji lake la fainali za Diamond League katika mbio za kuruka viunzi na maji mita 3,000.

Mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 21 alishangaza wakimbiaji nyota mwaka jana mjini Brussels baada ya kukimbia kwa dakika 9:02.36 na kunyakua taji lake la kwanza la Diamond League mbele ya bingwa wa Olimpiki Winfred Yavi wa Bahrain (9:02.87) na Muganda Peruth Chemutai (9:07.60). Yavi na Chemutai hawatakuwepo mjini Zurich, hali ambayo kocha wake Cherotich, Bernard Rono, anaamini inampa nafasi kubwa zaidi.

“Tumekuwa tukijifua kwa umakini tukilenga Mashindano ya Dunia yatakayofanyika Tokyo. Sasa macho yote yako kwa Faith, hasa kwa kuwa Yavi na Chemutai hawashiriki hapa,” alisema Kocha Rono.

“Yeye ni mtiifu, ana nguvu kisaikolojia, na tunawaheshimu wapinzani wote. Mashindano ya Zurich ni sehemu ya mpango mpana zaidi, na tuna matumaini mambo yatakuwa mazuri,” Rono aliongeza.

Rono, ambaye anasimamia kundi kubwa la wanariadha chipukizi katika Kambi ya Mafunzo ya Kalyet na Kalyet Global Sports Communication Camp huko Kipkelion, Kaunti ya Kericho, anasema mbio za Zurich ni jaribio muhimu kabla ya Tokyo.

“Ninashukuru Shirikisho la Riadha Kenya (Athletics Kenya), na pia ninatambua mchango wa makocha wote wa Team Kenya katika kuhakikisha wanariadha wetu wako imara. Tunatazamia kufanya vyema Tokyo, na ninawatakia wanariadha wote kila la heri,” alisema Rono.

Huko Zurich, Cherotich atakabiliana na bingwa wa dunia wa mwaka 2022 Norah Jeruto wa Kazakhstan, Marwa Bouzayani wa Tunisia, na Gabrielle Jennings wa Marekani miongoni mwa nyota wengine.

Cherotich tayari amekuwa na msimu mzuri wa Diamond League, akishinda mashindano mjini Doha, Oslo na Paris. Yavi ndiye pekee aliyemshinda mara moja msimu huu kwenye Prefontaine Classic huko Oregon, akimaliza kwa dakika 8:45.25 mbele ya Cherotich (8:48.71), huku Chemutai akimaliza wa tatu kwa 8:51.77.

Mchuano huo kule Oregon uliashiria kile kinachotarajiwa kuwa pambano kali zaidi kwenye Mashindano ya Dunia yajayo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending