Sports
Gor Yatimua Benchi La Kiufundi na Afisa Mkuu Mtendaji Wake
Kilabu ya Gor Mahia imevunjiliwa mbali kamati yake ya kiufundi ikiongozwa na kocha mkuu Zedekia ‘Zico’ Otieno kufuatia msimu mbovu wakiambulia patupu.
Mabingwa hao mara 21 wametaja hatua hiyo kuwa ni ya kujenga upya Kogalo baada kupoteza ligi ya taifa FKF kwa kilabu ya Kenya Police.
Wakufunzi washikilizi hao yani Otieno na Nam walipewa nafasi ya kunoa kogalo kwa muda baada ya kilabu hiyo kumtimua Raia wa Croatia Sinica Mihic kutokana na msururu wa matokeo duni.
Ni mara ya kwanza Kogalo kukosa kushiriki kimataifa huku nafasi hizo zikitwaliwa na Police ambao watashiriki ligi ya mabingwa barani Afrika CAF champions ligi na Nairobi United tajia la mashirikisho Barani Afrika CAF confederation.
Vile vile Mabingwa hao wazamani walitengaza kuachana na Afisa mkuu mtendaji Ray Oruo.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

