Sports
Harambee Stars Waahidi Ushindi Dhidi ya Burundi Kadri Safari ya Kombe la Dunia 2026 Inavyozidi Kupamba Moto
Timu ya taifa ya Harambee Stars imejaa kujiamini kabla ya mchezo wao muhimu wa kufuzu Kombe la Dunia la FIFA 2026 dhidi ya Burundi utakaochezwa Oktoba 9, 2025, huko Bujumbura.
Nahodha Michael Olunga alieleza matumaini yake kuhusu maandalizi na ari ya kupambana ya wachezaji, akisema timu imelenga kupata alama zote tatu.
“Wachezaji wengi tayari wamewasili. Tuna mtazamo chanya na kila mmoja yuko tayari kwa majukumu yaliyopo mbele yetu,” alisema Olunga.
Kocha mkuu Benni McCarthy alisisitiza maneno ya nahodha wake, akibainisha kuwa lengo la timu ni ushindi pekee.
“Hii ni nafasi yetu ya kupata alama tatu muhimu; tunajua kilicho hatarini tunapoingia kwenye pango la simba,” alisema McCarthy.
Kocha huyo alifafanua kuwa benchi la kiufundi limechambua mchezo wao wa awali dhidi ya Burundi na kufanya marekebisho ya kimkakati. Alibainisha kuwa huu si mchezo wa kulipiza kisasi, bali ni nafasi ya wachezaji kuonyesha vipaji vyao na uzalendo wao kwa taifa.
“Tunawaheshimu wapinzani wetu, lakini hiyo haimaanishi kwamba tutajizuia. Tunatumai wapinzani wetu wataingia uwanjani wakiwa na mtazamo huo huo,” aliongeza.
McCarthy pia alithibitisha kuwa wachezaji wengi waliitwa kwenye kikosi wamewasili, akiwemo mchezaji mpya Vincent Harper, ambaye mashabiki wengi wanataka kumuona akicheza kwa mara ya kwanza. Alisema kuna wasiwasi mdogo wa majeraha, lakini ana imani kuwa wachezaji wote watakuwa timamu ifikapo siku ya mechi.
Kenya sasa inalenga kuendeleza matokeo mazuri ya hivi karibuni na kutoa tamko thabiti huko Bujumbura, huku safari ya kuelekea Kombe la Dunia la 2026 ikizidi kupamba moto.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

