Sports
Harambee Stars Yaondoka Kuivaa Chad
Timu ya taifa Harambee Stars kushuka dimbani kucheza na Chad Juni 7,mechi hio ya kirafiki ikipigwa katika ardhi ya morocco kabla ya mechi ya pili juni 10.
Kwa mujibu wa kocha mkuu Benni McCarthy Mechi hizo mbili zitasaidia kikosi hicho kujinoa kwa mashindano ya CHAN mwezi Agosti humu nchini.
“Hizi ni mechi kwa mimi kupata nafasi ya kuwajua vyema wachezaji wangu lakini pia kujiandaa kwa ajili ya taji la Chan kwani hatutaki kuwa tu washiriki bali tunataka kuwa wapinzani pia.”
Kikosi kilichosafiri cha Stars ni pamoja na Magolikipa:
Brian Bwire,Farouk Shikhalo,Sepstanious Wekesa.
Mabeki; Brian Mandela,Alphonce Omija,Sylvester Owino,Siraj Mohammed,Abud Omar,Daniel Sakari,Swale Pamba na Lewis Banda.
Kiungo;Brian Musa,Alpha Onyango,Austine Odhiambo,Ben Stanley Omondi,Bonface Muchiri ,William Lenkupae,Adam Wilson ,James Kinyanjui na David Sakwa.
washambulizi;Beja Nyamawi,Moses Shuma na Emmanuel Osoro
Kiungo Mohammed Bajaber amejiondoa kutokana na jeraha.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

