Connect with us

News

Jopo la ushauri na Maimamu eneo la Takaungu lasisitiza Samuel Charo alisilimu kwa hiari yake

Published

on

Jopo la ushauri na maimamu katika eneo la Takaungu wadi ya mnarani kaunti ya Kilifi limepinga madai yalioibuliwa na wanafamilia wa kijana aliyeuawa baada ya kumuua na kula matumbo ya mzee mmoja aliyekuwa ustadh aliyetambulika kama Ainen.

Kwa mujibu wa ustadh Abubakar Ratili wa masjid Answar kule Takaungu, marehemu Samuel Kirao Charo alisilimishwa na kupewa jina Zakariyah akisisitiza kuwa marehemu alisilimu kwa hiyari yake mbele ya waislam wengine kwenye msikiti huo

Aidha Sheikh Mahadh Ali ambaye pia ni imam wa msikiti Maryam eneo hilo la Takaungu pamoja na Ustadh Mohamed Khamis wameeleza kuwa dini ya kiislam inaruhusu mwili kuzikwa usiku akikashifu swala la kuhusisha hatua hiyo na ushirikina kama ilivyodaiwa na baadhi ya watu.

Jopo hilo pia limeeleza kuwa wanafamilia walihusishwa ila walidinda kushirikiana nao jambo lililopelekea jamii hiyo ya kiislamu kuendeleza maziko ya marehemu kwa mujibu wa Imani ya dini ya kiislam.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Sakata ya mafuta yaathiri sekta ya uchukuzi nchini

Published

on

By

Huenda watumizi wa magari ya uchukuzi wa umma, wahudumu wa tuktuk na bodaboda wakalazimika kuongeza nauli kwa abiria kutokana na changamoto za ukosefu wa mafuta nchini na kuathiri zaidi shughuli za uchukuzi.

Hatua hii imetakana na changamoto za uhaba wa mafuta nchini baada ya kuibuka kwa sataka ya uagizaji wa mafuta ghushi kupitia bandari ya Mombasa.

Kulingana na serikali kupitia Wizara ya Kawi, sakata hiyo ya shilingi bilioni 12 ilikuwa imelata tani elfu 60 za mafuta ya petroli kinyume cha sheria pamoja na mipango ya serikali ya uagizaji mafuta wa serikali kwa serikali yaani G to G.

Sakata hii imepelekea Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya kudhibiti kawi na bei za mafuta nchini EPRA Daniel Kiptoo, Katibu katika Idara ya petroli nchini Mohammed Liban na mkurugenzi wa Kampuni ya Kenya Pipeline Joe Sang kujiuzulu.

Kujiuluzu kwao kumetokana na kukamatwa na maafisa wa idara ya upelelezi wa jinai nchini DCI, kwa ushirikiano na Tume ya maadili na kupambana na ufisadi nchini EACC baada ya kutilia shaka zabuni iliyopewa kampuni binafsi ya One Petroleum Limited inayomilikwa na mfanyibiashara mashuhuri jijini Mombasa.

Wahudumu wa sekta ya bodaboda wakikabiliwa na changamoto za uhaba wa mafuta ya Petroli

Siku ya Jumanne, Waziri wa Kawi nchini Opiyo Wandanyi alifanya kikao na wakurugenzi wa kampuni za mafuta nchini na kuagiza shehena ya mafuta katika bandari ya Mombasa kurejeshwa kwani serikali haitambua shehena hiyo.

“Wahusika wa sakata hiyo walikuwa na njama ya kuongeza bei ya mafuta nchini kwa shilingi 14 zaidi kwa lita wakitumia nafasi ya vita vinavyoendelea kati ya Iran na Marekani na Israel, hiyo hatuta kubali”, alisema Wandayi.

Hatua hiyo ilikuwa inalenga pia kukwepa mpango wa serikali wa uagizaji mafuta kutoka mataifa ya miliki za kiarabu wa serikali kwa serikali yaani G to Go, akisema wahusika wa sakata ya ufisadi ni lazima wachukuliwe hatua.

Itakumbukwa kwamba rais William Ruto hivi majuzi alidokeza kwamba wahusika wote wa sakata ya ufisadi kwenye sekta ya mafuta watachukuliwa hatua, akishililia kwamba serikali haitakubali ufisadi nchini, huku akikosa kuweka wazi hatma ya maafisa hao wakuu wa serikali.

“Hawa walaghai wa mambo ya mafuta watakipata, hawaweze kuhepa kwa sababu haiwezekani katika taifa letu la Kenya watu wanaone tuko na shida ya mashariki ya kati wanakuja kukoroga shida nyengine hapa Kenya, serikali itakabiliana kikamilifu na wafisadi”, alisema Rais Ruto.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Buriani Mama Dorothy Baya, 1947-2026

Published

on

By

Mwili wa Mama Dorothy Baya Mweri ambaye ni Mama mzazi wa bunge wa Kilifi Kazkazini Owen Baya umetolewa katika makafani ya hospitali ya rufaa ya Kilifi kaunti ya Kilifi.

Mwili wa Mama Dorothy umefanyiwa ibada fupi ya wafu nje ya makafani ya hospitali hiyo ikiongozwa na viongozi wa kidini kisha wananchi wakapata fursa ya kuutazama mwili ili kutoa heshima yao ya mwisho kwa marehemu.

Viongozi mbalimbali wa kisiasa pia walikuwa na nafasi ya kumpa mkono wa buriani Mama Dorothy wakiongozwa na Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro na Mwenyekiti wa bodi ya hazina ya michezo na sanaa ambaye pia ni mgombea wa wadhfa wa useneta kaunti ya Kilifi Wakili George Kithi.

Viongozi wengine waliokuwepo kutoa heshima zao za mwisho kwa Marehemu ni pamoja Mbunge wa Ganze Kenneth Tungule, Mbunge wa Kaloleni Paul Katana, Mgombea wa wadhfa wa uwakilishi wa kike kaunti ya Kilifi Christine Zawadi, miongoni mwa wengine.

Msafara wa Marehemu baadaye ulielekea katika kijiji cha Dabaso eneo bunge la Kilifi Kazkani kaunti ya Kilifi kwa ibada ya misa ya wafu katika Kanisa la St Stephen Dabaso kabla ya halfa ya mazishi siku ya Jumatatu.

Msafara wa Marehemu Mama Dorothy Baya ukielekea katika kijiji cha Dabaso eneo bunge la Kilifi Kazkani kaunti ya Kilifi kwa hafla ya mazishi.

Marehemu amewaacha watoto 6, akiwemo Mbunge wa Kilifi Kazikazini ambaye pia ni Naibu Kiongozi wa wengine bungeni Owen Baya, Askofu mkuu wa Kanisa la Kianglikana Dayosi ya Mombasa Alphonce Mwaro,Charity Mapenzi, Felix Mweri, Mercy Kadii na Catherine Harusi, pamoja na wajuu kadhaa.

Hata hivyo viongozi na wananchi wa tabaka mbalimbali wanatarajiwa kuhudhuria halfa ya mazishi ya Mama Dorothy itakayofanyika siku ya Jumatatu hapo kesho tarehe 6 mwezi Aprili mwaka huu katika kijiji cha Dabaso.

Mama Dorothy aliaga dunia tarehe 30 mwezi Machi, 2026.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending