Connect with us

News

Bajeti ya taifa yaongezeka hadi shilingi trilioni 4.6

Published

on

Huenda wakenya wakalazimika kuingia mifukoni mwao hata zaidi ili kugharamia bajeti ya taifa ya mwaka wa kifedha wa 2025/2026 ambayo inakadiriwa kufikia shilingi trilioni 4.6.

Bajeti hii imeongezeka na shilingi bilioni 363 kutokana na bunge la kitaifa kuidhinisha bajeti ya zaidi ili kukidhi mahitaji ya serikali licha ya bajeti ya mwaka wa kifedha wa 2024/2025 kuwa shilingi trilioni 4.3.

Japo wakenya wamekuwa wakilalamikia kupanda kwa gharama ya maisha wakiwa na matumaini ya kushuka kwa bajeti ya taifa ili kuwawezesha kukidhi mahitaji yao, matumaini hayo yameanza kupotea kutokana na mikakati ya kiuchumi iliyoidhinishwa na serikali ya Kenya kwanza.

Akizungumzia kuhusu ongezeko la bajeti hiyo kwa shilingi bilioni 363, Mwenyekiti wa Kamati ya bajeti katika bunge la kitaifa Samuel Atandi alisema fedha hizo za zaidi zitasaidia baadhi ya idara za serikali nchini ambazo zimekuwa zikikabiliwa na upungufu wa fedha.

Atandi ambaye pia ni mbunge wa Alego Usonga alidokeza kwamba sekta zilizoongezewa fedha ni pamoja na sekta ya Afya, Elimu na usalama wa taifa, akisisitiza kwamba suala hilo halifai kuchukuliwa kisiasa na badala yake litazamwe kama suala muhimu nchini.

Mwenyekiti wa Kamati ya bajeti katika bunge la kitaifa Samuel Atandi, akieleza bajeti ya taifa ya shilingi trilioni 4.6 ya mwaka wa kifedha wa 2025/2026

Kwenye ongezeko hilo la shiling bilioni 363, sekta ya afya nchini imeongezewa mgao wa shilingi bilioni 26, ambapo sasa itapata mgao wa shilingi bilioni 164, Tume ya huduma kwa walimu nchini TSC ikiongezewa shilingi bilioni 24 na kufikia shilingi bilioni 411, Idara ya usalama nchini ikiongezwa shilingi bilioni 53 na kufikia shilingi bilioni 418.

Hata hivyo kamati hiyo imeeleza wazi kwamba kwenye mgao wa idara ya usalama, shilingi bilioni 10 zitaelekezwa kwenye idara ya ujasusi nchini, shilingi bilioni 7.5 kwenye idara ya polisi na shilingi bilioni 24 kwa idara ya ulinzi nchini, ili kufanikisha usalama wa taifa.

Wakati huo huo Atandi alikiri kwamba wakenya watahusishwa kikamilifu katika kutoa maoni yao kuhusu mapendekezo ya bajeti hiyo ya shilingi trilioni 4.6 ya mwaka wa kifedha wa 2025/2026.

Kwa upande wake Waziri wa hazina ya kitaifa John Mbadi alisema wakenya watakuwa na fursa ya kutoa maoni yao kuhusu mapendekezo ya bajati hiyo ya taifa, akiwataka wanasiasa kujitenga na tabia ya kuchochea wakenya na kuvurugu masuala muhimu yanayohusu mwananchi.

Kulingana na kauli ya Kamati ya bajeti katika bunge la kitaifa, idara nyingi za kiserikali nchini zimekuwa zikitegemea kipengele cha 223 cha Katiba kuitisha fedha za dharura bila idhinisho la bunge la kitaifa na kwamba hatua hiyo imeonyesha wazi utumizi mbaya wa raslimali za umma.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending