Sports
Junior Strikers Mabingwa Wa Afrika Mchezo wa Voliboli
Kikosi cha voliboli cha wanawake chipukizi wasiozidi umri wa miaka 20, maarufu kama Junior Strikers, kimetwaa ubingwa wa Mashindano ya Afrika kwa Chipukizi yaliyokamilika jana mjini Yaoundé, Cameroon.
Hii ni baada ya warembo hao kuwalaza wenyeji Cameroon kwa seti 3–1 katika fainali kali iliyopigwa jana mjini humo.
Junior Strikers walishinda kwa seti za 26–24, 19–25, 28–26 na 25–16, na hivyo kulipiza kisasi baada ya kupoteza mechi moja pekee dhidi ya wenyeji hao katika hatua ya mzunguko.
Mchezaji nyota Terry Tata Mallin alitajwa kuwa mchezaji bora wa mashindano, huku akishinda pia tuzo ya mchezaji bora wa mchezo dhidi ya timu za Misri, Senegal, Burundi na Uganda.
Mchezaji wa nafasi ya nje Milka Akinyi naye alituzwa kama mchezaji bora wa kuzuia mashambulizi ya wapinzani.
Mashindano hayo, yaliyodumu kwa wiki moja, yalihusisha mataifa ya Cameroon, Kenya, Uganda, Burundi, Misri na Senegal.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

