Sports
Kenya Mabingwa Afrika, Kombe La Catchball
Kikosi cha Taifa cha Kenya mchezo wa Catchball ndiyo mabingwa wa Afrika kombe hilo lililotamatika mjini Soweto Afrika Kusini mwishoni mwa Juma.
Mashindano hayo ambayo ni ya akina dada yalingoa nanga Juni 14-21 yalikua yanajumuisha mataifa ya Kenya,Uganda,Ghana na Afrika Kusini yakilenga kuimarisha mchezo huo katika ukanda wa Afrika kwa jumla.
Kulingana na Rais wa mchezo huo Papa Douglas Shilubane akiwashukuru timu zote za kigeni kwa kuitikia mwito ametaja kuwa lengo lao ni kufanya mchezo wenyewe ujulikane barani.
“Tunalenga kuhahakisha mchezo huu unaenea kote Barani Afrika na kukuja kwenu ni hatua mwafaka wa kuendeleza mchezo huu tulionza hapa Afrika kusini na kueneza kote Barani.”
Kenya ilishinda mechi zake zote tano ambazo alishiriki na hivyo basi kutawazwa kuwa bingwa wa makala hayo ya kwanza.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

