Sports
Kenya yamaliza ya pili Duniani katika Riadha Mjini Tokyo,Japan
Kenya imemaliza ya pili kwenye msimamo wa medali huku makala ya 20 ya mashindano ya Riadha Duniani yakikamilika Jumapili mjini Tokyo,Japan.
Kenya iliyokuwa ikiwakilishwa na wanariadha 58 imezoa jumla ya medali 11,dhahabu 7 fedha 2 na shaba 2.
Beatrice Chebet alinyakua dhahabu mbili (5000 na 10,000),Faith Kipyegon(1500m) Emmanuel Wanyonyi (800m)Faith Cherotich(3000msc) na Peres Jepchirchir (Marathon).
Washindi wa nishani za fedha walikuwa Faith Kipyegon mita 5000 na Dorcas Ewoi mita 3000 kuruka viunzi na maji huku Edmund Serema akinyakua shaba ya mita 3000 kuruka viunzi na maji na Raynold Cheruiyot mita 1500.
Aidha Wakenya walivunja rekodi tatu za mashindano hayo wakiwa Emmanuel Wanyonyi,Faith Cherotich na Lilian Odira.
Marekani ilitwaa ubingwa kwa medali 16 za dhahabu fedha 5 na shaba 5.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

