Connect with us

Sports

Kikosi cha Wanamichezo wa Para ya Kenya kinazidi kujiandaa kwa Mashindano ya Dunia Yakayofanyika Mjini New Delhi,India

Published

on

Kikosi cha Wanamichezo wa para kutoka Kenya hawachi jambo lolote kwa bahati nasibu wanapojiandaa kwa Mashindano ya Dunia yatakayofanyika mwezi huu mjini New Delhi, India.

Timu hiyo ilifanya mazoezi ya nguvu  katika Uwanja wa Kimataifa wa Moi, Kasarani, ambapo makocha walizingatia kuboresha mbinu na kuongeza kujiamini kabla ya kivumbi cha kimataifa.

Mazoezi hayo yaliwaleta pamoja wanamichezo wa fani mbalimbali ikiwemo mitupo na mbio fupi za uwanjani wote wakiwa na hamu ya kupeperusha bendera ya Kenya kwenye jukwaa la dunia. Kikao hicho kilisisitiza uimara, mbio za kasi, na maandalizi ya kisaikolojia, huku makocha wakiwahimiza wanamichezo kudumisha nidhamu na hali bora ya mwili kadri siku ya mashindano inavyokaribia.

“Tunafanya kazi katika kasi, uimara, na zaidi ya yote nguvu ya kisaikolojia,” alisema Kocha Mkuu Henry Kirwa, akiongeza: “Tunawaomba Wakenya wote wawatie moyo wanamichezo hawa — iwe kazini, mgahawani, au ukiwa nyumbani. Mshikamano wenu unamaanisha kila kitu na utawasukuma kutoa walicho nacho bora kabisa.”

Kwa wanamichezo wengi, mashindano haya ni nafasi ya kurekebisha makosa ya nyuma na kutoa matokeo bora zaidi katika ulingo wa dunia.

“Hadi sasa mazoezi yamekuwa mazuri kama mnavyoona. Mwaka huu hautakuwa kama mingine, mwaka huu utajaa medali,” alisema mtoaji wa tufe, Rajab Chetty.

“Lengo langu ni kuwa wa kwanza na kuleta heshima nyumbani, kama mtoaji wa tufe wa kwanza katika kipengele cha F11. Nataka kuweka historia,” aliongeza.

Mwanariadha wa mbio fupi T47, Stency Neema, naye alisisitiza: “Kambi ni nzuri, tunajiandaa vizuri. Tunaamini tutafanya vyema… safari hii tumejiandaa kikamilifu.”

Maafisa wa timu nao walieleza matumaini kwamba Kenya itatoa matokeo mazuri mjini New Delhi, ikijenga juu ya sifa inayoongezeka ya nchi katika michezo ya para.

“Tumejiandaa kwa dunia, tegemeeni mambo makubwa na tutaliletea taifa fahari. Tegemeeni medali nyingi,” alisema Rais wa KNPC, Ronald Milare.

Timu itaendelea na maandalizi yake maeneo mbalimbali nchini katika siku zijazo, kabla ya kusafiri kwenda New Delhi Septemba 24 kwa ajili ya kuzoea mazingira kabla ya mashindano — yatakayoanza rasmi Septemba 27.

Kwa kuwa wanamichezo bingwa wa para kutoka duniani kote wanatarajiwa kushiriki, tukio hilo litakuwa jaribio kubwa kwa kikosi cha Kenya.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending