Connect with us

Sports

Kikosi kipya cha Bayern Kupata Mtihani Mpya Kilabu bingwa dhidi ya Chelsea, siku ya Jumatano.

Published

on

Haya Ni kama marudio ya fainali ya mwaka 2012 uwanjani Allianz Arena, ambapo Chelsea walishinda kwa mikwaju ya penalti. Bayern haina muda wa kutulia baada ya msimu wa joto uliojaa mabadiliko makubwa, hasa safu ya ushambuliaji.

Washambuliaji Leroy Sane, Kingsley Coman, Thomas Mueller na Mathys Tel wote waliondoka majira ya joto. Ni wachezaji wawili pekee waliokuja: Luis Diaz kutoka Liverpool na Nicolas Jackson kutoka Chelsea kwa mkopo. Kwa kuwa Jamal Musiala na Alphonso Davies wako nje kwa majeraha ya muda mrefu, ukosefu wa usajili mpya ulichochea ukosoaji nadra kutoka kwa nyota wa timu, Harry Kane.

Muingereza huyo mwenye umri wa miaka 32, ambaye si maarufu kwa kutoa kauli tata, alisema kikosi cha Bayern ni “chembamba”, akiongeza: “pengine ni miongoni mwa vikosi vidogo zaidi ambavyo nimewahi kuwa navyo katika maisha yangu ya soka.”

Akiwa na mabao manne na pasi mbili za mabao katika mechi tano za kwanza, Diaz ameanza kwa kasi nchini Ujerumani.

Lakini Chelsea, waliotwaa ubingwa wa Kombe la Dunia la Vilabu baada ya kuilaza Paris Saint-Germain miezi miwili tu iliyopita, huenda wakawa na mtihani mkubwa zaidi.

Kama Chelsea, Bayern wanatarajiwa kuvuka hatua ya makundi, lakini wanataka kufuzu moja kwa moja na kuepuka michezo ya mtoano ya nyongeza.

Mwaka jana, Bayern walimaliza nafasi ya 12 na walihangaika kumfunga Celtic, wakishinda kwa jumla ya 3-2.

Kane alikiri Jumamosi kwamba mzigo wa ziada uliwapunguzia kasi mwishoni mwa msimu:
“Ni muhimu kuwa kwenye nane bora kwa sababu mchezo wa ziada unaweza kuleta tofauti kubwa. Mwaka jana, tulipocheza na Celtic nyumbani na ugenini wakati wa kipindi chetu cha kazi nyingi, kulikuwa na tofauti kubwa, na tukapoteza wachezaji wachache baada ya kipindi hicho cha Machi. Ni muhimu kuanza vizuri.”

Zaidi ya miaka 13 tangu Chelsea iwashinde Bayern katika uwanja wao wa nyumbani, timu zote mbili zimefanikiwa kutwaa taji jingine la Ligi ya Mabingwa.

Kuondoka kwa Mueller majira ya joto kumemwacha nahodha Manuel Neuer kama mchezaji pekee wa zamani kati ya timu zote mbili atakayecheza Jumatano.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending