Connect with us

Sports

Kiungo Eze Eberechi Aangamiza Spurs Tena Arsenal wakirejea katika mbio za Ubingwa

Published

on

Kiungo wa Arsenal, Eberechi Eze, aliiumiza tena Tottenham baada ya kufunga mabao mawili yaliyosaidia vinara hao wa Ligi Kuu ya England kuifunga Tottenham mabao 4-1 katika dabi ya kaskazini mwa London Jumapili.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilimaliza msururu wa mechi mbili bila ushindi na kujitanua kileleni kwa tofauti ya pointi tano dhidi ya Manchester City walioko nafasi ya pili. Mbali na mabao ya Eze, mshambuliaji Viktor Gyokeres pia alifunga mabao mawili katika ushindi huo mkubwa.

Baada ya kukataa kujiunga na Tottenham msimu uliopita, Eze ameonekana kung’ara zaidi akiwa katika jezi ya Arsenal hasa dhidi ya wapinzani hao wa jadi. Gyokeres naye alituliza presha mapema kipindi cha pili, kabla Eze hajafunga bao la tatu na Gyokeres kukamilisha ushindi huo muhimu.

Kwa Gyokeres, aliyekuwa na msimu mgumu baada ya kuhamia kutoka Sporting Lisbon, mabao hayo yalikuwa ya ukombozi mkubwa, sawa na ilivyokuwa kwa Eze.

Arsenal walikuwa wameanza kuyumba katika mbio za ubingwa baada ya sare dhidi ya Brentford na Wolves, matokeo yaliyofufua matumaini ya Manchester City. Ushindi wa City wa mabao 2-1 dhidi ya Newcastle ulikuwa umepunguza pengo hadi pointi mbili kabla ya dabi hiyo.

Kocha Arteta aliwahimiza wachezaji wake kuvumilia presha ya mbio za ubingwa, akisema yeyote asiyeweza kustahimili “kelele na mashambulizi” bora aondoke klabuni na kuwaachia wengine waandike historia yao wenyewe.

Hata hivyo, licha ya ushindi huo, hatma ya ubingwa bado iko mikononi mwa Manchester City. Iwapo kikosi cha Pep Guardiola kitashinda mechi zake zote 11 zilizosalia, kitachukua taji hilo bila kujali matokeo ya Arsenal katika mechi zao 10 zilizobaki.

Arsenal sasa hawajapoteza katika dabi nane zilizopita dhidi ya Tottenham. Mashabiki wao walifurahia ushindi huo huku wakikumbusha wapinzani wao kuwa hakuna uhakika wa kukutana tena msimu ujao.

Tottenham wako pointi nne tu juu ya eneo la kushuka daraja, huku wakiongeza idadi ya mechi bila ushindi hadi tisa katika mchezo wa kwanza wa kocha wa muda Igor Tudor baada ya Thomas Frank kutimuliwa.

Ingawa Tudor ana uhakika kwa asilimia mia moja kuwa klabu hiyo itasalia Ligi Kuu, hatari ya kushuka daraja bado ni tishio baada ya kushinda mechi mbili pekee katika 18 zilizopita.

Arsenal walitangulia kufunga dakika ya 32 baada ya Pape Sarr kupoteza mpira karibu na lango lao. Bukayo Saka alimchezea krosi Eze aliyepiga voli safi kutoka umbali wa yadi 10 na kufunga bao la kwanza.

Hata hivyo, uongozi huo ulidumu kwa dakika mbili tu baada ya kosa la Declan Rice kupokonywa mpira nje kidogo ya eneo la hatari, Kolo Muani akafunga kwa shuti kali lililomshinda kipa David Raya.

Kipindi cha pili kilianza kwa presha kutoka Arsenal, na dakika ya 47 Jurrien Timber alimpa pasi Gyokeres aliyepata nafasi kutokana na uzembe wa safu ya ulinzi ya Tottenham na kupiga shuti kali lililomshinda kipa Guglielmo Vicario.

Eze alifunga bao la tatu dakika ya 61 baada ya makosa mengine ya ulinzi wa Spurs, akitumia vyema mpira uliomkuta ndani ya eneo la hatari.

Gyokeres alihitimisha ushindi huo dakika za majeruhi kwa kufunga bao la nne huku mashabiki wa Tottenham wakianza kuondoka uwanjani kwa huzuni.

Ushindi huo umeirejesha Arsenal katika mstari wa mbele wa mbio za ubingwa huku Tottenham wakizidi kusukumwa kuelekea hatari ya kushuka daraja.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Sports

Bingwa wa dunia mbio za mitaa 1500 Faith Kipyegon ateuliwa kuwania tuzo za kila mwaka za ‘Laureus World Sportswoman of the Year.’

Published

on

By

Nyota wa mbio za masafa ya kati kutoka Kenya, Faith Kipyegon, amepata uteuzi wake wa tatu mfululizo kuwania tuzo ya Mwanamichezo Bora wa Kike wa Mwaka katika hafla maarufu ya Laureus World Sports Awards, hatua inayozidi kuthibitisha ubabe wake katika kizazi hiki cha wanariadha.

Tuzo hizo, zinazotambuliwa kimataifa kama “Oscars za Michezo”, huandaliwa na Laureus Sport for Good Foundation na hulenga kutambua mafanikio ya kipekee, uthabiti na mchango chanya wa michezo duniani.

Uteuzi wa Kipyegon kwa miaka mitatu mfululizo unaonyesha si tu kipaji chake, bali pia uimara wa kiwango chake cha juu kwa muda mrefu. Mwaka 2024 aliteuliwa baada ya msimu wa kihistoria wa 2023 ambapo alivunja rekodi tatu za dunia na kushinda dhahabu mbili katika Mashindano ya Dunia.

Mwaka 2025 alirejea tena kwenye orodha ya wateule kufuatia mafanikio makubwa katika Michezo ya Olimpiki ya Paris, ambako aliweka historia kwa kuwa mwanamke wa kwanza kushinda medali tatu za dhahabu mfululizo katika mbio za mita 1,500.

Sasa mwaka 2026, anawania tuzo hiyo tena baada ya kuvunja rekodi yake mwenyewe ya dunia ya mita 1,500 na kutwaa taji lake la nne la dunia katika msimu bora wa 2025.

Katika kinyang’anyiro cha mwaka huu, Kipyegon anakutana na ushindani mkali kutoka kwa nyota wengine wa kimataifa akiwemo Sydney McLaughlin-Levrone, Melissa Jefferson-Wooden, Aitana Bonmati, Aryna Sabalenka, na Katie Ledecky.

Uteuzi huu unaendeleza hadhi ya Kipyegon kama mmoja wa wanariadha bora zaidi duniani na fahari kubwa kwa Kenya katika jukwaa la kimataifa.

Continue Reading

Trending