Connect with us

Sports

Klabu ya Soka ya Ulinzi Stars, inayoshiriki Ligi Kuu ya Kenya (KPL), Jumatatu imefuta kazi kocha mkuu Dunstan Nyaudo

Published

on

Klabu ya Soka ya Ulinzi Stars, inayoshiriki Ligi Kuu ya Kenya (KPL), Jumatatu ilimfuta kazi kocha mkuu Dunstan Nyaudo kufuatia msururu wa matokeo mabaya katika ligi hiyo ya juu.

Mabingwa wa zamani wa KPL walitangaza katika taarifa kwamba kocha huyo ameachishwa majukumu yake “mara moja.”

“Uongozi unathamini kujitolea, taaluma na huduma ya Kocha Nyaudo kwa timu, ndani na nje ya uwanja, wakati wote akiwa madarakani.
Tunamshukuru kwa dhati kwa mchango wake kwa familia ya Ulinzi Stars na tunamtakia mafanikio mema katika safari yake ijayo,” ilisomeka sehemu ya taarifa hiyo.

Timu hiyo ya wanajeshi imekuwa na msimu mgumu, ikishinda mechi moja pekee kati ya tano walizocheza hadi sasa. Wako nafasi ya 13 kati ya timu 18 kwenye msimamo wa ligi, wakiwa na pointi 5 kutokana na michezo hiyo mitano.

Uamuzi huo unamaliza kipindi cha tatu cha Nyaudo kama kocha mkuu wa timu hiyo ya kijeshi, ukifunga sura nyingine katika uhusiano wake wa muda mrefu na Ulinzi Stars.

Akiwa mchezaji kati ya mwaka 1993 na 2002, Nyaudo alikuwa mmoja wa mabeki waliochezea Ulinzi mechi nyingi zaidi na alikuwa muhimu katika kuibua vipaji vipya wakati wa uchezaji wake.

Mwaka 2017, aliteuliwa kwa mara ya kwanza kama kocha wa muda kabla ya kuthibitishwa rasmi mwaka 2018, lakini akaondoka mwaka 2020 baada ya matokeo mabaya.

Alirejea tena Julai 2024 baada ya kipindi cha mafanikio na timu ya vijana chini ya miaka 20 (U20), ambako alisaidia kulea vipaji chipukizi.

Hata hivyo, licha ya juhudi zake za kujenga upya kikosi cha wakubwa, Ulinzi Stars walimaliza msimu wa 2024/25 katika nafasi ya 12.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending