Connect with us

Sports

Kocha Domenico Tedesco Kocha mpya Fernabache ,Akichukua nafasi ya Jose Mourinho

Published

on

Kocha wa zamani wa Ubelgiji Domenico Tedesco amechukua nafasi ya Jose Mourinho kama meneja wa klabu ya Uturuki Fenerbahce kwa mkataba wa miaka miwili, klabu hiyo ya Istanbul ilitangaza Jumanne.

“Kocha wetu mpya ni Domenico Tedesco,” Fenerbahce walitangaza kupitia X, wakiongeza kuwa kocha huyo wa Kiitaliano-Kijerumani atasaidiwa na nahodha wa zamani wa timu hiyo Gokhan Gonul.

Tedesco, mwenye umri wa miaka 39, aliifundisha Ubelgiji kuanzia Februari 2023 hadi alipofutwa kazi Januari mwaka huu. Awali, aliwahi kuifundisha Schalke, Spartak Moscow na RB Leipzig.

Mreno Mourinho alifutwa kazi Agosti 29 baada ya klabu kushindwa kufuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, ikipoteza kwa Benfica kwenye mechi za mchujo.

Matarajio yalikuwa makubwa wakati kocha huyo mwenye umri wa miaka 62 aliwasili Istanbul miezi 14 iliyopita.

“Hakuna ahadi. Lakini ni wazi kuwa lengo kuu, ndoto kuu ni kushinda Ligi Kuu ya Uturuki,” alisema kocha huyo aliyewahi kushinda Ligi ya Mabingwa Ulaya mara mbili.

Hata hivyo, alishindwa kutimiza ndoto yake ya kumaliza ukame wa mataji uliyoikumba klabu hiyo bingwa mara 19 tangu mwaka 2014.

Kocha huyo wa zamani wa Chelsea, Real Madrid, Inter Milan, Manchester United, Tottenham Hotspur na Roma aliiongoza timu ya njano ya Istanbul kufika nafasi ya pili msimu uliopita nyuma ya Galatasaray.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending