Sports
Kocha Domenico Tedesco Kocha mpya Fernabache ,Akichukua nafasi ya Jose Mourinho
Kocha wa zamani wa Ubelgiji Domenico Tedesco amechukua nafasi ya Jose Mourinho kama meneja wa klabu ya Uturuki Fenerbahce kwa mkataba wa miaka miwili, klabu hiyo ya Istanbul ilitangaza Jumanne.
“Kocha wetu mpya ni Domenico Tedesco,” Fenerbahce walitangaza kupitia X, wakiongeza kuwa kocha huyo wa Kiitaliano-Kijerumani atasaidiwa na nahodha wa zamani wa timu hiyo Gokhan Gonul.
Tedesco, mwenye umri wa miaka 39, aliifundisha Ubelgiji kuanzia Februari 2023 hadi alipofutwa kazi Januari mwaka huu. Awali, aliwahi kuifundisha Schalke, Spartak Moscow na RB Leipzig.
Mreno Mourinho alifutwa kazi Agosti 29 baada ya klabu kushindwa kufuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, ikipoteza kwa Benfica kwenye mechi za mchujo.
Matarajio yalikuwa makubwa wakati kocha huyo mwenye umri wa miaka 62 aliwasili Istanbul miezi 14 iliyopita.
“Hakuna ahadi. Lakini ni wazi kuwa lengo kuu, ndoto kuu ni kushinda Ligi Kuu ya Uturuki,” alisema kocha huyo aliyewahi kushinda Ligi ya Mabingwa Ulaya mara mbili.
Hata hivyo, alishindwa kutimiza ndoto yake ya kumaliza ukame wa mataji uliyoikumba klabu hiyo bingwa mara 19 tangu mwaka 2014.
Kocha huyo wa zamani wa Chelsea, Real Madrid, Inter Milan, Manchester United, Tottenham Hotspur na Roma aliiongoza timu ya njano ya Istanbul kufika nafasi ya pili msimu uliopita nyuma ya Galatasaray.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

