Sports
KOCHA ERIK TEN HAG RAIA WA UHOLANZI APIGWA KALAMU NA BAYER LEVERKUSEN
Mkufunzi wa zamani wa Manchester United Erik Ten Hag ametimuliwa na klabu ya Bayern Leverkusen baada ya mechi tatu pekee akiinoa klabu hiyo ya taifa la Ujerumani.
Kocha huyo raia wa uholanzi aliteuliwa na klabu hiyo ya Bundesliga mwezi Mei akiichukua nafasi ya Xabi Alonso, ambaye aliondoka kuinoa Real Madrid ya uhispania.
Hata hivyo, amekuwa na mwanzo mgumu wa maisha nchini Ujerumani, akikusanya pointi moja pekee katika mechi zake mbili za mwanzo.
Leverkusen walipoteza mchezo wao wa kwanza 2-1 wakiwa nyumbani dhidi ya Hoffenheim licha ya kupata bao la mapema kupitia kwa beki wa zamani wa Liverpool, Jarell Quansah.
Hatua ya kumtimua imekuja baada ya timu hiyo kutupilia mbali uongozi wa 3-1 ugenini Jumamosi dhidi ya wachezaji 10 wa Werder Bremen na kutoka sare ya 3-3.
Akizungumza baada ya kukatishwa tamaa Jumamosi, Ten Hag aliiambia Sky: ‘Wachezaji hawako tayari tuna timu mpya na baadhi ya wachezaji hawako fiti vya kutosha kucheza. Timu haikufanya vizuri hata kidogo wakati wa hatua ya mwisho ya mchezo. Ndivyo ilivyo. Wanahitaji kuleta nguvu zaidi na kuwa fiti zaidi ili kufikia viwango vyangu.’
Hata hivyo mchezaji nyota Florian Wirtz, Jeremie Frimpong, Jonathan Tah na Granit Xhaka ni miongoni mwa wachezaji muhimu zaidi ya nusu dazeni walioondoka Leverkusen majira ya joto.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

