Connect with us

Sports

Kocha Nuno Espírito Santo Atimuliwa Nottingham Forest Baada ya Michezo Mitatu Pekee ya Msimu Mpya

Published

on

Mkufunzi Nuno Espírito Santo ametimuliwa na Nottingham Forest baada ya michezo mitatu pekee ya msimu mpya.

Kocha huyo kutoka Ureno aliiongoza Forest kufuzu Ulaya msimu uliopita kwa mara ya kwanza katika karne hii, lakini uhusiano wake na viongozi wa klabu hiyo ulikuwa umedorora sana majira haya ya kiangazi.

Nuno aliikosoa hadharani sera ya usajili ya Forest na kukiri kuwa uhusiano wake na mmiliki Evangelos Marinakis haukuwa mzuri kama ulivyokuwa msimu uliopita. Nuno, ambaye alijiunga na Forest mwezi Desemba 2023, pia alihangaika kufanya kazi chini ya mfumo mpya ambapo afisa mkuu wa zamani wa Arsenal, Edu, aliteuliwa kuwa mkuu wa masuala ya soka kilabuni humo. Marinakis siku chache zilizopita alikuwa amepuuzilia mbali madai ya mgongano kati yake na kocha wake.

Katika taarifa iliyotolewa saa 6:15 asubuhi hii leo, Forest ilisema: “Nottingham Forest Football Club inathibitisha kwamba, kufuatia hali za hivi karibuni, Nuno Espírito Santo ameondolewa majukumu yake kama kocha mkuu.”

Na licha ya kuiletea klabu hiyo mafanikio makubwa uwanjani, Marinakis na kocha wake wa zamani hawakuwa wakikubaliana mara zote.

Hali hiyo ilidhihirika mapema msimu uliopita wakati mmiliki wa Forest aliingia uwanjani moja kwa moja katika uwanja wa City Ground kumkemea kocha wake baada ya sare ya 2-2 dhidi ya Leicester City.

Na dhahiri bado hawajayamaliza tofauti zao, kwani mwezi uliopita Nuno alikiri kwa uaminifu mkubwa kwenye mkutano na wanahabari kwamba uhusiano wao ulikuwa “sio mzuri.”

Kauli hiyo ilizua tetesi kuwa Marinakis angeweza kumfuta kazi kocha huyo wa zamani wa Wolves, huku kukiwa na fununu za kumhusisha na Ange Postecoglou, au hata Nuno mwenyewe kujiuzulu – jambo ambalo alilipinga vikali.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending