Sports
Kocha Wa Stars Benni Mccarthy ataja Kikosi cha CHAN
Mkufunzi wa timu ya Taifa ya Soka Harambee Stars Benni Mccarthy amekitaja kikosi cha wachezaji 30 kuanza kambi ya mazoezi kwa makala ya CHAN Agosti 3-Agosti 30 katika mataifa ya Kenya,Uganda na Tanzania.
Magolikipa:
Faruk Shikhalo (Bandari), Sebastian Wekesa (Kariobangi Sharks), Brian Opondo (Tusker FC)
Mabeki;
Siraj Mohammed (Bandari FC), Manzur Suleiman (KCB), Pamba Swaleh (Bandari FC), Abud Omar (Kenya Police),Alphonce Omija (Gor Mahia), Sylvester Owino (Gor Mahia), Michael Kibwage (Tusker), Daniel Sakari (Kenya Police), Lewis Bandi (AFC Leopards), Kevin Okumu (KCB)
Viungo;
Brian Musa( Kenya Police), Kelly Madada (AFC Leopards), Keith Imbali (Shabana), Alpha Onyango (Gor Mahia), Mathias Isogoli (KCB), Staphod Odhiambo (Ulinzi Stars), Austine Odhiambo (Gor Mahia), Ben Stanley (Gor Mahia)
Washambulizi;
Mohammed Bajaber (Kenya Police), Boniface Muchiri (Ulinzi Stars), David Sakwa (Bandari), Emmanuel Osoro (FC Talanta), Yakeen Muteheli (Ulinzi Stars), Edward Omondi (Sofapaka), Ryan Ogam (Tusker),Moses Shummah (Kakamega Homeboyz), Beja Nyamawi (Bandari)
Stars wanafungua kampeini yao dhidi ya DR.Congo uwanjani Kasarani Agosti 3.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

