Connect with us

Sports

KOMBE LA TRIATHLON AFRIKA 2025 KUANDALIWA KILIFI

Published

on

Kikosi cha Wanariadha 20 wa Kenya kiko tayari kwa changamoto ya Kilifi huku wapinzani wa bara wakisaka pointi za viwango

Pwani ya Kenya itageuka tena kuwa uwanja wa uhodari na ustahimilivu wakati nchi inapoandaa toleo la 7 la Kombe la Afrika la Duathlon na Triathlon wikiendi hii mjini Kilifi.

Mashindano hayo yanashirikisha wanariadha kutoka nchi 11 zikiwemo Japani, Ujerumani, Venezuela, Moroko, Mauritius, Austria, Hungaria, Israeli, Tanzania, Singapore, na Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Kwa upande wa Timu ya Kenya, kikosi cha wanariadha 20 kinachojumuisha wachezaji wa kiwango cha juu, vijana, na wale wa makundi ya umri (age group) kitaiwakilisha nchi katika mashindano hayo ya siku mbili yaliyopangwa kufanyika Jumamosi na Jumapili.

Mashindano hayo yana umuhimu mkubwa kwani yanabeba pointi muhimu za kufuzu kwa Olimpiki na Mashindano ya Dunia.

Mwaka jana, Kenya ilifanya historia kwa kuandaa Kombe la Duathlon kwa mara ya kwanza, na toleo la mwaka huu lililopanuliwa linaimarisha nafasi yake kama mwenyeji muhimu katika kalenda ya michezo ya uvumilivu barani Afrika.

Nahodha wa wanaume Joseph Okal ataongoza mashambulizi ya Kenya katika kipengele cha duathlon. Akizungumza kabla ya mashindano, alisema:

“Tumefanya mazoezi vizuri na timu imejaa motisha. Vipindi vyetu vya mazoezi vimekuwa na mpangilio na vinaendeleza uthabiti wetu. Hiyo inatupa nguvu na uvumilivu tunaposhuka Pwani.”

Okal, aliyeshinda dhahabu katika Kombe la Afrika la Duathlon 2024 Kasarani kwa muda wa 1:02:01, anaamini umoja wa timu na faida ya uwanja wa nyumbani vinaweza kuleta tofauti.

“Kucheza nyumbani kunatupa ujasiri,” alisema.
“Ni kweli, kuna presha — lakini ni presha nzuri, inayokusukuma kutoa uwezo wako wote. Kama nahodha, ninazingatia timu kwanza. Tunashindana kama kitu kimoja, na kila mstari wa kumalizia ni ushindi wa pamoja.”

Nahodha wa timu ya wanawake Bernice Kariuki, ambaye pia anashiriki kwenye triathlon, alikubaliana naye.

“Kwa mazoezi ya mbio ninatumia uwanja wa Strathmore, na kwa kuendesha baiskeli napendelea eneo la Limuru kwa sababu ya urefu wake — inakufanya uwe na nguvu zaidi unaposhindana karibu na usawa wa bahari,” alisema.
“Ili kufanya vizuri, lazima ujue kukabiliana na presha. Kuwa nyumbani kunatupa motisha ya ziada kuiwakilisha nchi yetu kwa fahari.”

Miongoni mwa washiriki wa juu wa Kenya ni Megan Irungu, anayerejea kwenye triathlon baada ya kumaliza kwa muda wa 1:26:14 katika mashindano ya msimu uliopita.

Kariuki pia alibainisha kuwa Kenya imekuwa ikifanya vizuri katika makundi yote kwenye mashindano ya karibuni.

“Kwa wachezaji wa makundi ya umri, tulipata nafasi kadhaa za juu kati ya wakubwa na vijana,” alisema.
“Hii inaonyesha ukuaji na uthabiti wa mpango wetu wa maendeleo.”

Kwa upande wa ufundi, Kocha Camilla Lydia ameongoza vikosi vya duathlon na triathlon kwa msisitizo wa nidhamu, mazoezi ya mwili, na uwezo wa kubadilika.

“Hii ni timu changa lakini yenye nidhamu,” alisema.
“Wameitikia vyema mafunzo, na tunalenga katika mabadiliko ya haraka, unywaji maji, na urejeshaji nguvu. Kushindana na wanariadha wa kimataifa kunawapa uzoefu muhimu. Tunapenda kushukuru serikali ya Kenya kupitia Wizara ya Michezo kwa msaada mkubwa kwa mashindano haya.”

Mashindano ya Kilifi — ambayo yamefanyika mfululizo kwa miaka saba tangu kuanzishwa kwake mwaka 2021 — yanaendelea kukua kwa hadhi, yakitoa fursa kwa wanariadha kutoka Afrika na maeneo mengine kupima uwezo wao, kupata pointi za viwango, na kuonyesha maendeleo ya bara hili kwenye mchezo huo.

“Kama timu, tunataka kufanya vizuri, kujifunza, na kuiwakilisha Kenya kwa njia bora zaidi,” alisema Okal.
“Kila mwendo wa baiskeli, kila hatua, kila kuogelea kuna maana. Hii ni safari ya kuiweka Kenya kwenye ramani ya dunia ya triathlon.”

“Wachezaji wamefanya mazoezi vizuri na wako na ari kubwa. Wamejiandaa kwa viwango vinavyohitajika katika mashindano yote mawili. Tunapenda kushukuru serikali ya Kenya kupitia Wizara ya Michezo kwa msaada mkubwa katika mashindano haya.”

Kombe la Afrika la Duathlon litafanyika Jumamosi, Oktoba 11, likifuatiwa na Kombe la Afrika la Triathlon siku ya Jumapili, Oktoba 12, likiandaliwa na Triathlon Kenya, Africa Triathlon, na World Triathlon.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending